Friday, April 18, 2014

CHELSEA wana imani kuwa beki wao mkongwe, John Terry atakubali kusaini mkata mwingine utaomfanya awepo mpaka msimu ujao, amesema kocha msaidizi Steve Holland ijumaa hii.

Beki huyo wa zamani wa timu ya Taifa ya England ameripotiwa kupewa ofa ya mkataba mpya, lakini mshahara wake utakuwa nusu ya mshahara apatao sasa.

Hata hivyo, Holland amegoma kuzungumzia makubaliano na beki wao huyo mwenye miaka 33, wakati huo huo akieleza kuwa wakongwe wengine, Frank Lampard na Ashley Cole wapo mbioni kusaini mikataba mipya.

“John amekuwa na msimu mzuri; ameifanya beki yetu iwe katika kiwango bora na yeye amekuwa akifanya kazi hiyo”.

“Najua John anataka kubaki Chelsea na Chelsea inamhitaji John, kwahiyo nadhani makubaliano yatafikiwa wiki chache zijazo”.

“Kama ilivyo kwa John, naye Lampand na Cole watapewa heshima hiyo. Hawa ni wachezaji wa muda mrefu hapa klabuni na nadhani tunawapa heshi makubwa”. Alisema Holland katika mkutano na waandishi wa habari kuelekea mechi ya kesho dhidi ya Sunderland.


Chelsea kwasasa wapo katika nafasi ya pili kwenye  msimamo, pointi mbili nyuma ya Liverpool wenye pointi 77 kileleni.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video