Na Baraka Mpenja, Dar es salaam
KIUNGO matata wa Mbeya City fc, Steven Mazanda
ataendelea kuitumikia klabu yake hiyo msimu ujao wa ligi kuu soka Tanzania bara
kutokana na kubakiwa na mwaka mmoja katika mkataba wake.
Mazanda ameuambia mtandao huu kuwa bado anadaiwa
na klabu yake na kwa bahati mbaya malengo yake hayakutimia msimu uliopita baada ya kuishia nafasi ya tatu katika
msimamo.
“Kitu kikubwa ni maslahi. Lakini sidhani kama
Mbeya City watashindwa kunipa kile ninachohitaji”.
“Nimesikitishwa sana na timu yangu kushika nafasi
ya tatu. Tulikuwa na malengo ya ubingwa, lakini haijatokea”.
“Mechi zote za mwisho sikucheza kwasababu ya
majeruhi ya mguu wangu wa kulia, nadhani nitakuwepo msimu ujao kuendeleza
harakati”. Alibainisha Mazanda.
Hata hivyo, Mazanda aliongeza kuwa kwasasa
anaendelea kujitibu mguu wake wakati huu wa likizo.
“Ninaendelea na matibabu ya mguu wangu. Hali sio
mbaya kwasasa kwasababu napiga mazoezi mepesi mepesi ili kujiimarisha afya
yangu”. Alisema Mazanda.
Mazanda ambaye ni chaguo la kwanza katika nafasi
ya kiungo namba nane kwa kocha Juma Mwambusi hakusita kuwashauri vijana wa
Mbeya City fc kuwa maslahi ni kitu cha kwanza katika mpira, lakini waangalie
sana aina ya timu zinazowahitaji.
“Unaweza kutoka Mbeya City ukaenda klabu nyingine
kwa kufuata maslahi, lakini ukakosa nafasi ya kucheza”
“ Ni vizuri kufikiria vizuri unapoamua kuondoka
ili usije kumaliza soka lako”.
“Siogopi kucheza timu nyingine kwasababu ukijituma
unapata namba. Cha msingi tujipange vizuri”. Alisema Mazanda.
0 comments:
Post a Comment