Sunday, April 27, 2014



Na Baraka Mpenja, Dar es salaam
BEKI wa kushoto wa zamani wa Yanga SC, timu ya taifa ya Tanzania, Taifa stars na sasa maafande wa Ruvu Shooting, Stephano Mwasyika amewashauri vijana wanaochipukia katika soka kuiga mambo waliyofanya kaka zao na kubuni mbinu mpya ili walisaidie taifa siku za usoni.
Katika mahojiano maalum na mtandao huu, Mwasyika amesema akiwa Stars 2010 walichukua ubingwa wa CECAFA Senior  Challenge Cup, lakini vijana wanatakiwa kujituma zaidi ili kufika mbali kwasababu taifa lina uchu wa kupata mafanikio.
“Ukiangalia uongozi wa sasa wa TFF, nadhani kuna kitu wamekiona mbeleni ndio maana wanawekeza nguvu kwa vijana”
“ Timu itaweza kufanya vizuri miaka ya 2017-18, lakini kwasasa si rahisi kwasababu vijana wanatakiwa kuaminiwa na kupewa muda wa kutosha”. Alisema Mwasyika.
Mwasyika amewataka watu kuwapa moyo wachezaji wanaochipukia ili kuwajenga zaidi.
“Wachezaji wanaochipukia hawajawa sawa kisaikolojia. Anaweza kucheza vizuri mechi hii nyingine akachemsha”.
“ Kinachotakiwa kufanyika ni kmshauri na kuwatia moyo, lakini anapotokea mtu anawapa kashifa inawaharibu na kuwaondoa mchezoni”. Aliongeza Mwasyika.
Hata hivyo akaenda mbali zaidi na kuwashauri wadogo zake kuwa katika mpira kuna changamoto kubwa, hivyo wasiwe wepesi wa kukata tamaa kwa sababu ya maneno ya watu.
Beki huyo aliongeza kuwa kila mchezaji anataka kucheza timu ya taifa ili baadaye aende kimataifa.
“Angalia mfano akina Samata, Ulimwengu ambao sasa wamefika mbali kiasi”.
“Kwasasa wamekuwa wazoefu kwasababu wamecheza mechi nyingi za kimataifa. Vijana waige mfano wao. Kikubwa wafanye kazi yao kwa bidii na kutosikilza maneno ya watu. Alisema Mwasyika.
Aidha, Mwasyika amewashauri viongozi kutambua kuwa mpira wa miguu huwa unabadilika, kuna wakati mchezaji anaweza kucheza vizuri na kuna wakati ukamkataa.
“Watu wameshakariri kuwa Tanzania  kuna kuuza mechi. Vitu kama hivyo vipo, mimi sikatai. Lakini kuna wakati mwingine viongozi wanawapa lawama wachezaji  bila kujua kitu”.
“Unaposikia mtu kauza mechi na unaanza kuzungumza lazima uwe na uhakika”.
“Siku hizi kuna mitandao, kama mtu ametumiwa hela unaweza kujua tu ukifuatilia. Utajua kuna hela ilitumwa kutoka kwa mtu fulani kwenda kwa mtu fulani”.
“Viongozi wa siku hizi wanatengeneza kama majungu fulani kwenye timu. Utasikia fulani kauza mechi, lakini hawana uthibitisho. Timu ikifungwa utasikia mechi imeuzwa, mara marefaa wamenunuliwa, lazima tuwe tunafuatilia zaidi”. Alisema Mwasyika.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video