Na Baraka Mpenja, Dar es salaam
CHAMA cha soka mkoani Mbeya, MREFA, kimeendelea
kujivunia mafanikio ya kuaminiwa na shirikisho la soka Tanzania TFF kwa
kuziweka timu za Taifa mkoani Mbeya.
Mwenyekiti wa MREFA, Elias Mwanjala ameuambia mtandao
huu kuwa kuwekwa kambi ya maboresho ya Taifa stars mjini Tukuyu ilikuwa fursa
nzuri kwa wafanyabiashara na wapenzi wa soka mkoani humo kuiona timu yao.
Mwanjala aliushukuru uongozi wa TFF chini ya rais
Jamal Malinzi kwa kuendelea kuwapa fursa muhimu kama hizo na hasa baada ya
kuamua mchezo wa kirafiki wa kimataifa kati ya Taifa Stars na Malawi kufanyika
mkoni humo.
“TFF wanajua juhudi zetu. Uwanja wa Sokoine
ulikuwa mbaya sana, lakini tumeuboresha kwa nguvu zote na sasa mechi ya
kirafiki ya Taifa stars inafanyika katika uwanja huu. Hii ni heshima kubwa kwa
MREFA”.
“Kwasasa tunajenga vyumba vya kubadilishia nguo
vyenye hadhi ya kimataifa. Dhamira yetu ni kuwa na uwanja bora zaidi weye hadhi
kubwa”. Alisema Mwanjala.
Taifa stars chini ya Kocha mpya,
Mart Nooij aliongeza wachezaji tisa katika kikosi kilichochapwa mabao 3-0 na
Burundi siku ya maadhimisho ya miaka 50 ya muungano wa Tanganyika na Zanzibara,
aprili 26 mwaka huu uwanja wa Taifa.
Wachezaji hao waliongezwa kwa ajili
ya mechi ya kirafiki dhidi ya Malawi (The Flames) itakayochezwa Mei 4 mwaka huu
katika Uwanja wa Sokoine jijini Mbeya.
Wachezaji walioongezwa ni Edward
Charles Manyama (JKT Ruvu), Elias Maguli (Ruvu Shooting), Hassan Dilunga
(Yanga), Hussein Javu (Yanga), John Bocco (Azam), Kelvin Friday (Azam), Oscar
Joshua (Yanga), Nadir Haroub (Yanga) na Shomari Kapombe (AC Cannes, Ufaransa).
Kwasasa Stars ipo kambini mjini Tukuyu na siku
mbili kabla ya mechi hiyo itarudi mjini Mbeya tayari kwa maandalizi ya mwisho.
Akizungumzia timu za Prisons na Mbeya City fc,
Mwanjala alisema zimejitahidi kupambana msimu uliopita wa ligi kuu ingawa
zimeishia maeneo tofauti.
“Mbeya City tulianza kupotea baada ya kufungwa na
Yanga, Coastal na mwisho Azam fc”.
“Timu haikuwa na uzoefu, lakini msimu ujao
tutakuwa mabingwa kwasababu tutakuwa wazoefu”.
“Kwa Prisons kidogo uzoefu mdogo walionao
umewabakisha ligi kuu, kikubwa ni kuziandaa timu hizi ili msimu ujao zifike
mbali”.
“Prisons ilipoteza kete zake mzunguko wa kwanza,
lakini raundi ya pili ilicheza soka zuri sema bahati haikuwa yao.” Alisema
Mwanjala.
Mwenyekiti huyo aliongeza kuwa wanajitahidi kuisaidia
timu nyingine ya Kimondo fc ili iingie ligi kuu.
“Tuna imani
Kimondo fc itaweza kupanda ligi kuu, lakini kumbuka tuna timu nyingie ya Wenda
fc, mabingwa wa mikoa”
“Wanaenda kushiriki ligi ya
mabingwa wa mikoa, tunaamini itafuzu kucheza ligi daraja la kwanza”. Aliongeza Mwanjala.
0 comments:
Post a Comment