Sunday, April 20, 2014


Ally  Mayay Tembele
Ally Mayay (wa pili kushoto kwa waliochuchumaa) enzi zake akiichezea Yanga SC
Na Baraka Mpenja, Dar Es Salaam
BEKI na nahodha wa zamani wa Yanga SC, Ally Mayay Tembele amewaasa viongozi, wachezaji na mashabiki wa klabu za ligi kuu soka Tanzania bara kutambua kuwa mpira wa miguu ni mchezo wa makosa.
Akihojiana na mtandao huu  Mayay alisema wachezaji wanapokosea wanabebeshwa lawama na kupata hukumu kubwa ikiwemo kusimamishwa na klabu zao.
“Mpira wa miguu ni mchezo wa makosa. Ili mchezaji afunge goli, lazima mchezaji pinzani afanye makosa. Huwezi kufunga goli kama mpinzani wako hajakosea”.
“Kwa bahati mbaya Watanzania wengi tunaangalia mpira wa Ulaya kwa jicho lingine na mpira wa Tanzania kwa jicho lingine. Anapofanya kosa Ferdinand au David Luiz kwa wenzetu wanachukulia kawaida”.
“Wanatambua kuwa makosa ni sehemu ya mchezo. Lakini akifanya kosa hilo kwa mfano Yondani, Mosoti au mchezaji yeyote, kwetu utaambiwa kapewa rushwa. Ifike muda nasisi tusiwahukumu sana wachezaji”. Alisema Mayay.
Mayay aliongeza kuwa maneno mengi ya wachezaji kuuza mechi yanaanzia kwa mashabiki wa soka na kwa habati mbaya viongozi nao wanayabeba kama yalivyo.
“Kiongozi unaposikia mchezaji wako kahongwa, usibebe kama yalivyo, lazima kwanza ujiridhishe mwenyewe kwa kutafiti.”
“Halafu ukumbuke kuwa makosa huwa yapo katika mchezo. Baada ya hapo amua sasa atakavyo”. Alisema Mayay.
Akizungumzia ligi ya msimu huu, Mayay alisema ilikuwa nzuri na ya ushindani mkubwa hususani kwa nafasi ya ubingwa.
‘Binafsi nilifurahishwa sana na kasi ya Mbeya City fc, imeifanya ligi iwe bora na yenye mvuto. Hawa jamaa wameifanya ligi kuwa maarufu na kuzungumzwa sana”.
‘Sishangazwi na Azam fc kutwaa ubingwa. Tayari kwa misimu miwili walishika nafasi ya pili. Walichokuwa wanakitafuta msimu huu ni ubingwa. Wamekuwa bora na waliwekeza sana. Nadhani wamestahili”.
“Msingi wa Azam fc ulijengwa na kocha Muingereza Sterwart John Hall na alipokuwa anaondoka alimuandikia mrithi wake Joseph Omog kila kitu. Hakika alimpa njia nzuri na Omog alikuja kumalizia kazi ya  Sterwart”.
“Omog amekuwa muungwana sana kwasababu amekubali kuwa mafanikio yake yamechangiwa kwa kiasi kikubwa na Sterwart”. Alisema Mayay.
Kuelekea msimu mpya wa 2014/2015, Mayay alisema anatarajia ligi nzuri zaidi ya msimu huu kwasababu kumekuwepo na ongezeko la timu za wananchi.
‘Sina hakika, lakini nadhani Ndanda fc na Stand United zinaweza kufanya vizuri msimu ujao. Najua wananchi wanaozizunguka klabu hizi wameiga mfano wa watu wa Mbeya. Nafikiri itakuwa ngumu kwa timu nyingine kutoka na pointi tatu maeneo ya Shinyanga na Mtwara”.
“Natarajia ligi bora zaidi ya msimu huu. Udhamini nao umekuwa mzuri kwasasa”.
Ligi kuu ya Tanzania bara pazia lake limefungwa jana kwa Azam fc kutwaa ubingwaa baada ya kufikisha pointi 62.
Mbali na kutwaa ubingwa huo, Azam fc haijawahi kufungwa mchezo wowote msimu huu.
Yanga wameambulia nafasi ya pili kwa pointi zao 56, huku Mbeya City wakiwa wa tatu kwa pointi 49.
Wekundu wa Msimbazi Simba wamemaliza na pointi 38 katika nafasi ya nne.
JKT Oljoro, Rhino Rangers na Ashanti United zimeshuka daraja na kuzipisha timu za Ndanda fc ya Mtwara, Stand United ya Shinyanga na Polisi Morogoro ya mkoani Morogoro.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video