Antony Matogolo mwenye jezi namba 16 mgongoni wakati wa mechi yao na Azam fc uwanja wa sokoine jijini Mbeya
Na Baraka Mpenja, Dar es salaam
KIUNGO wa ulinzi wa Mbeya City fc, Antony Matogolo
amebainisha kuwa kama timu yoyote itamhitaji na kumhakikishia maslahi mazuri
anaweza kuondoka katika klabu yake hiyo iliyotikisa soka la Bongo msimu
uliopita.
Akizungumza na mtandao huu, Matogolo amesema mpira
ni maisha yake na inapotokea sehemu yenye maslahi mazuri zaidi hana budi
kwenda.
“Kwa upande wangu mimi, soka ni maisha, halafu ni
kazi. Hata wewe kwenye kazi yako inapotokea mtu mwingine mwenye maslahi mazuri
anakuhitaji, haina budi kwenda sehemu unayoona itakusaidia zaidi”.
“Ni kweli naipenda timu yangu, naiamini, nawaamini
viongozi wake na walimu wanaonifundisha, bado nina mkataba na Mbeya City fc”.
“Siwezi kusema nitaondoka kwa sasa hivi, lakini
ikitokea, ninaweza kuangalia sehemu nyingine yenye maslahi mazuri”. Alisema
Matogolo.
Matogolo amebainisha kuwa inapotokea mchezaji anatoka
klabu moja kwenda nyingine anakutana na changamoto kwasababu anakutana na watu
wengine na makocha tofauti, lakini kwa upande wake kikubwa ni kupambana.
“kuhama sio lazima, kwasababu unatakiwa kuangalia,
je, huko ninakoenda nitapa nafasi na kuendelea kutumika”.
“ Kwahiyo unapotaka kuhama lazima uangalie vitu
vingi zaidi ya maslahi”. Alisema Matogolo.
Kiungo huyo aliyepanda hewani aliongeza kuwa yeye
anaweza kucheza timu yoyote ile.
“Kwa mfano wanavyocheza Azam fc hawawezi kucheza
kama Mbeya City kwasababu ina wachezaji tofauti na makocha tofauti wenye
falsafa tofauti”.
“Lakini ukijipa muda wa kujifunza unaweza kuendana
na mfumo mpya”. Alisema Matogolo.
Aidha, mtaalum huyo wa kutibua mipango ya
wapinzani kueleka eneo lao la hatari alisema kwasasa anaendelea na mazoezi ya
kawaida kuendelea kujiweka fiti.
“Mazoezi ninayofanya kwasasa ni tofauti na
ninapokuwa na klabu yangu. Kwasasa naweza kufanya mara moja kwa siku na
kuendelea na shughuli nyingine”.
“Nakutana na watu wengine ninaokaa nao mtaani,
lakini mazoezi si makali sana” Alisema Matogolo.
Akizungumzia nafasi ya tatu waliyoshika msimu huu,
Matogolo alisema walistahili kwasababu ya uchanga wao japokuwa malengo yao
hayakutimia.
“Ulikuwa msimu wetu wa kwanza, changamoto zilikuwa
nyingi. Lakini tutakuja tena na mashabiki waendelee kutuamini”. Alihitimisha
Matogolo.
0 comments:
Post a Comment