Friday, April 18, 2014

azam bingwa
Na Baraka Mpenja, Dar Es Salaam
MABINGWA Azam fc wanatarajia kuandika historia hapo kesho kwa kutwaaa taji bila kupoteza mechi yoyote ambapo watakabiliana na JKT Ruvu katika uwanja wa Azam Complex, Uliopo Chamazi, nje kidogo ya jijini la Dar es salaam.
Hii itakuwa mechi ya mwisho kwa Azam fc waliocheza mechi 25 mpaka sasa bila kufungwa.
Kocha mkuu wa klabu hiyo, Mcameroon, Joseph Marius Omog alisema kutwaa ubingwa ni mafanikio makubwa, lakini kuchukua mwari bila kufungwa mechi yoyote ni historia nzuri kwa klabu.
“Wachezaji wangu wasibweteke na ubingwa. Bado tuna mechi moja kesho dhidi ya JKT Ruvu. Nahitaji kushinda mchezo huo ili kuweka rekodi nzuri”.
“Tutaingia kwa nguvu zote na kuhakikisha tunawafunga wapinzani wetu”. Alisema Omog.
Naye kocha mkuu wa JKT Ruvu Fredy Minziro alisema kikosi chake kimejiandaa kukabiliana na Azam fc kwa nguvu.
“Tunafahamu kuwa Azam fc ni timu bora msimu huu. Hajafungwa mechi yoyote na wanahitaji kujenga historia kupitia sisi”.
“Tumejiandaa vizuri na kizuri ni kuwa tumenusurika kushuka daraja. Nilishasema toka awali kuwa malengo yetu ilikuwa kukwepa kushuka daraja na hivi sasa tumeweza. Tunamshukuru Mungu na tunamuomba atuongoze vyema hapo kesho”. Alisema Minziro.
Msimu huu umekuwa mzuri mno kwa Azam fc kwani toka mzunguko wa kwanza walicheza kwa mafanikio wakiwa chini ya kocha mkuu, Sterwat John Hall.
Baada ya Hall kujiuzulu mwishoni mwa mzunguko wa kwanza, Mcameroon Omog alichukua nafasi yake na kuendeleza rekodi ya kutofungwa.
JKT Ruvu wapo nafasi ya 9 kwa pointi 31 baada ya kucheza mechi 25, hivyo wapo mikono salama kabisa.
Azam fc wamecheza mechi 25 na kujikusanyia pointi 59 kileleni, huku tayari wakiwa mabingwa kwasababu hakuna klabu yoyote inayoweza kuzifikia pointi hizo.
18 Apr 2014

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video