Thursday, April 17, 2014

Na Baraka Mpenja, Dar Es Salaam
0712461976

YANGA SC wenye machungu ya kupoteza ubingwa wao msimu huu baada ya kuwasili jana jioni kutoka Arusha wameamua kutuliza akili yao katika hoteli ya Landmark, Kunduchi, jijini Dar es Salaam ili kujiwinda dhidi ya Simba sc jumamosi uwanja wa Taifa.

Mnyama Simba yeye ameamua kutuliza bunduki zake muhimu huko visiwani Zanzibar ambako walienda jana.

Yanga angalau wameambulia nafasi ya pili msimu huu baada ya kucheza mechi 25 na kujikusanyia pointi 55 kibindoni,.

Simba wao hali ni tete kwasababu wamepata nafasi ya nne kufuatia kushuka dimbani mara 25 na kujikusanyia pointi 37 katika nafasi ya nne, lakini kila timu ina mchezo mmoja mkononi.

Abdallal Kibadeni anayeifundisha Ashanti United kwasasa aliiongoza Simba katika mchezo wa mzunguko wa kwanza na kufanikiwa kutoka sare ya 3-3 akianza kufungwa mabao 3-0 kipindi cha kwanza.

Kipindi cha pili aliwatuliza vijana wake na kufanikiwa  kusawazisha mabao yote matatu na kuleta shida upande wa pili.

Baada ya mechi hiyo, Kibadeni na msaidizi wake, Jamhuri Kiwhelu `Julio` walitimuliwa kwa sababu ya timu kufanya vibaya mzunguko wa kwanza wakati ilianza kwa kuongoza ligi.

Makocha wa Simba na Yanga wanakuwa hatarini kupoteza kazi zao pindi timu hizi zinapokaribia kukutana.

Kuna idadi kubwa ya makocha waliotumiliwa kwa Simba kuifunga Yanga au Yanga kuifunga Simba sc.

Kumbuka Ernie Brandts aliwapa Yanga ubingwa, lakini sare ya 3-3 na kipigo cha desemba 21 mwaka jana  katika mechi ya `Nani Mtani Jembe` kiliotesha nyasi kibarua chake baada ya kufungwa mabao 3-1.

Brandts alishutumiwa na uongozi wa Yanga na mashabiki kuwa ameshusha kiwango cha klabu hiyo, lakini ukweli unabaki kuwa ni matokeo ya kipigo na sare aliyoyapa kutoka Simba.

Viongozi wa timu hizi mbili zenye uhasimu mkubwa huwa hawana masihara pale kocha waliyemwajiri anashindwa kumfunga  mtani.

Ukiwa kocha wa Yanga unaweza kuwa mikono salama ukifungwa na Mgambo au Azam fc, lakini kufungwa na Simba sc ni hatari sana, hata kwa upande wa Simba ni hivyo hivyo.

Kibadeni alitimuliwa na mikoba yake kuchukuliwa na Mcroatia Dravko Logarusic, huku kiungo wa zamani na nahodha wa Simba, Suleiman Abdallah Matola, `Veron` akirithi nafasi ya kocha msaidizi iliyokuwa chini ya Julio.

Logarusic ana ajira ya miezi sita katika klabu yake na hatima ya kibarua chake bila shaka imebakia katika mechi ya jumamosi.

Kocha huyu hajawahi kuonja machungu ya kufungwa na Yanga kwasababu tangu aanze kazi aliwafunga Yanga katika mechi ya `Nani Mtani Jembe`.

Sasa anaiongoza Simba iliyowajeruhi mashabiki wake kwa matokeo mabaya msimu huu dhidi ya Yanga iliyokosa ubingwa.
Mechi hii ni ya heshima kwa Simba sc na  Yanga kwasababu wote wamekosa ubingwa mbele ya Azam fc.

Mtihani huu ni mkubwa mno kwa Logarusic , japokuwa yeye anasema hana presha kabisa kwasababu ni mechi ya kulinda heshima tu kwake.

Loga anasema anatambua mechi hii inazikitanisha klabu zenye historia kubwa nchini, lakini hana shaka kabisa kwani ataweza kufanya vizuri.

Ukija kwa upande wa Yanga, `Nani Mtani Jembe` ilimkosesha kibarua Mholanzi, Ernie Brandts na msaidizi wake, Fredy Minziro na kazi zao kuchukuliwa na Mholanzi mwenzie, Hans Van Der Pluijm na Mtanzania Charles Mkwasa.

Pluijm hajawahi kukutana na presha ya mechi ya watani wa jadi, lakini viongozi wa klabu wamemueleza umuhimu wa mechi hiyo.

Pluijm anasema anajiandaa kufanya vizuri dhidi ya Logarusic anayeonekana kuichukuliwa kirahisi mechi hiyo.

Pluijm naye ana ajira ya miezi sita kama ilivyo kwa Loga na tayari ameshawakosesha ubingwa Yanga.

Kilichobaki kwake ni kulinda heshima ya klabu kwa kuwafunga Simba jumamosi.

Mkwasa anaujua utamaduni wa klabu hizi mbili na lazima amemshauri Pluijm kuweka mikakati mizito kwasababu kufungwa inaweza kuleta matatizo katika kazi yake.

Plujm arejee nyuma ili kufahamu  mambo yalivyokuwa mechi ya mzunguko wa kwanza ambayo mwenzake  alitoka sare ya 3-3 na Yanga kufungwa 3-1 `Nani Mtani Jembe` .

Baada ya matokeo hayo, atagundua kuwa Yanga wanahitaji kujipunguzia machungu ya kukosa ubingwa kwa kuwafunga Simba sc, kwa maana hiyo ili kukwepa yaliyomkuta Brandts lazima ajipange vizuri.

Loga na Pluijm watakutana kwa mara ya kwanza katika mchezo huo hapa nchini na atakayeshinda atakuwa na uhakika wa ajira ya mkataba mpya.

Loga alipoteza mchezo wa mwisho dhidi ya Pluijm walipokuwa Ghana ambako Loga alikuwa akiifundisha Hearts Of Oak, huku Pluijm akiwa na Berekum Chelsea ambapo Pluijm alishinda mabao 4-2.

Je, kati ya Logarusic  na Pluijm nani kupata mkataba mpya jumamosi?


Hili ni swali litakalojibiwa baada ya dakika 90 za mchezo wa watani wa jadi ndani ya dimba la Taifa jijini Dar es salaam.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video