Friday, April 25, 2014



JURGEN Klopp amesema ana `sababu 1,000` za kuendelea kubaki Borussia Dortmund na kukataa kujiunga na Manchester United.
Klopp amekuwa akihusishwa kuhamia Old Trafford tangu David Moyes atimuliwe jumatatu ya wiki hii, lakini kocha huyo amekanusha tetesi hizo.
Pia kocha huyo ameongeza kuwa hana mawasiliano yoyote na viongozi wa juu wa Man United.
“Ni jambo baya kumkataa mtu kabla hajatuma ombi, lakini haiwezekani” Klopp amewaambia waandishi wa habari.
Klopp aliyewahi kuifundisha Mainz kabala ya kujiunga na Dortmund mwaka 2008, alisaini mkataba mpya mwezi oktoba mwaka jana ambao utamfanya akae Signal Iduna Park hadi mwaka 2018.
Kocha huyo, 46, amekiri kuwa klabu ya Man United ni kubwa, lakini hana mpango wa kwenda.
“Kuna sababu zaidi ya 1,000 za mimi kuwa na furaha zaidi na klabu yangu”. Alisema Klopp.
Dortmund wanakabiliana na Bayer Leverkusen leo katika uwanja wa Bay Arena,  mechi ya ligi kuu nchini Ujerumani, Bundesliga, huku wakiwa nafasi ya pili na wapo nyuma kwa pointi 17 dhidi ya mabingwa Bayern Munich.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video