Sunday, April 20, 2014

MENEJA wa Liverpool, Brendan Rodgers  baada ya ushindi wa leo wa mabao 3-2 dhidi ya Nowrich amemsifia mshambuliaji wake kinda,  Raheem Sterling na kusema ndiye mchezaji bora zaidi kijana barani Ulaya.
 
Sterling amefunga mabao mawili leo kati ya matatu na kuifanya Liverpool ishinde mechi 11 mfufulizo na kuukaribia ubingwa baada ya miaka 24 kupita bila taji.
Pia alitoa pasi kwa Luis Suarez na kumfanya  afunge bao lake la 30 msimu huu.
“Nadhani ni mchezaji bora zaidi kijana kwa mpira wa Ulaya, kwa upande wangu, nadhani ingekuwa chini ya miaka 21. Kiukweli nimefurahishwa na kuimarika kwake. Anatumia muda wake mwingi katika kazi yake”.
“Tumejitahidi kumchezesha nafasi tofauti ili kuongeza uwezo wake. Ni mtoto mwenye akili sana”.
Liverpool wameongezwa morali baada ya kipigo cha jana cha Chelsea na sasa wanahitaji pointi saba tu katika mechi tatu zilizosalia dhidi ya Chelsea, Crystal Palace na Newcastle.
Akizungumzia changamoto ya ubingwa, Rodgers alisema: “ Ninapenda ushindani ulivyo mkubwa. Nimefanya kazi kwa muda mrefu nikiwa kocha kijana”.
“ Tangu nimeingia katika kazi hii nina miaka 15. Malengo yangu kama kocha ni kuwaweka wachezaji kuwa bora zaidi na matokeo yake ni kushinda”.
“Kuishi Liverpool ni faraja na heshima kwangu. Najua wachezaji wananipatia ninachotaka, nimeshinda mechi 11 mfululizo, haya ni mafanikio kwangu”. Amesema Rodgers.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video