Friday, April 25, 2014



KOCHA wa timu ya taifa ya Brazil Luiz Felipe Scolari anaamini Atletico Madrid itaitupa nje Chelsea katika michuano ya UEFA msimu huu.
Chelsea ilitoa suluhu ya bila kufungana na Ateletico katika mchezo wa kwanza wa nusu fainali katika dimba la Vicente Calderon jumanne ya wiki hii, na kumuweka Jose Mourinho katika nafasi ya kufanya vizuri wiki ijayo dimba la Stamford Bridge.
Hata hivyo, Scolari amesema Chelsea itatolewa, huku sababu zake zikiwa za ubinafsi zaidi.
Kocha huyo anaiombea mabaya Chelsea  isifuzu fainali mei 24 mwaka huu ili wachezaji wake tegemeo David Luiz, Oscar, Willian na Ramires wapate muda wa kupumzika
“Kwetu itakuwa vizuri kwa Atletico kuwatoa Chelsea, kwasababu itawapa wachezaji wangu wanne fursa ya kupumzika”. Scolari amewaambiwa waandishi wa habari.
Scolari amethibitisha kuwa beki wa Chelsea, Luiz atakuwa moja ya wachezaji wa kikosi cha kwanza katika michuano ya kombe la dunia majira ya kiangazi mwaka huu nchini kwao Brazil.
“Wachezaji niliowachagua kuwa viongozi ni David Luiz, Julio César na Fred," .
“Nimeshawachagua tayari na nimekuwa nikizungumza nao mara kwa mara”
“Sina wasiwasi na orodha ya mwisho ya kikosi changu, lakini nitasubiri ligi ziishe”.
Scolari amesisitiza kuwa hana wasiwasi juu ya Neymar ambaye ni majeruhi kwasasa kwasababu anaamini atakuwepo katika fainali za mwaka huu licha ya kutokuwa na msimu mzuri FC Barcelona.
“Neymar atakaribishwa vizuri timu yake ya taifa. Sijali ukosoaji wa Kihispania juu ya mchezaji huyu”.
“Tunajua klabu yake haina mafanikio kwa sasa, lakini Brazil ina aina yake ya uchezaji wa mpira, hivyo Neymar atakuwepo”.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video