MSHAMBULIAJI hatari wa Atletico Madrid, Diego
Costa anaamini kuwa Chelsea hawatatumia mbinu yao ya kujilinda katika mchezo wa
nusu fainali ya pili ya UEFA hapo kesho uwanja wa Stamford Bridge.
Jose Mourinho alitumia mbinu ya `Kupaki basi`
katika mechi ya kwanza uwanja wa Vicente Calderon na kulazimisha suluhu ya bila
kufungana na alitumia mbinu kama hiyo kuwafunga Liverpool mabao 2-0 jumapili
iliyopita katika mchezo wa ligi.
Hata hivyo, Costa mwenye uraia wa Hispania
anatarajia kuona Chelsea ikishambulia zaidi katika mechi ya kesho jumatano kwa
malengo ya kufika fainali.
“Sina shaka, ni mchezo mkubwa, acha tufurahi na
kuucheza”. Costa amewaambia waandishi wa habari.
“Itakuwa meci tofauti kwa wenyeji, watajitahidi
kucheza kwa kushambulia zaidi”.
Atletico msimu huu wana uchu wa kutwaa ubingwa wa
La Liga tangu walipofanya hivyo kwa mara ya mwisho mwaka 1996 na Costa ana
ndoto ya kubeba kombe Calderon.
“Ninataka kushinda kombe la ligi na itakuwa furaha
kubwa kufanya hivyo mbele ya mashabiki wetu tutakapokutana na Malaga”.
Aliongeza.
Atletico Madrid katika mechi bili za mwisho
watasafiri kuwafuata Levante na mchezo wa kufungia msimu watakutana na Malaga
nyumbani.
0 comments:
Post a Comment