Sunday, April 20, 2014

Na Baraka Mpenja, Dar es salaam


COASTAL UNION maarufu kwa jila `Wagosi wa Kaya` hawajajitendea haki kumaliza katika nafasi ya 9 kwenye msimamo wa ligi kuu soka Tanzania bara msimu huu.

Wakicha chini ya kocha Mkenya, Yusuf Chipo, Costal wamefanikiwa kukusanya pointi 29 tu katika michezo 26 waliyocheza msimu huu.

Wamefanikiwa kushinda mechi 6 tu, sare 11 na kufungwa mechi 9.

Jana katika mechi ya mwisho walipokea kichapo cha bao 1-0 kutoka kwa Kagera Sugar katika uwanja wao wa Mkwakwani.

Coastal ni mjoa ya timu iliyofanya maandalizi makubwa msimu huu na kusajili wachezaji wazuri.

Waliwekeza fedha nyingi katika kikosi chao na kuweka kambi nzuri kwa wachezaji wao.

Kumbuka wakijiwinda na mzunguko wa pili, walienda kuweka kambi nchini Oman ambako walicheza mechi za kirafiki.

Wakati wakiwa Oman, Yanga walikuwa zao Uturuki kujiandaa na mzunguko wa pili.

Haya ni maandalizi makubwa sana kwa klabu, hivyo walistahili kushika nafasi tatu za juu.

Yanga ya Uturuki imeshika nafasi ya pili kwa pointi 56, huku Azam fc walioenda Afrika kusini kujiandaa kabla ya ligi kuu msimu huu kuanza wakimaliza na pointi 62 kileleni na kuwa mabingwa wapya.

Mbeya City waliomaliza nafasi ya tatu kwa pointi 49, wao walikaa zao mwakareli Tukuyu kwa muda mrefu.

Simba nao walifanyia maandalizi hapahapa nchini, kama ilivyo kwa klabu nyingi za ligi kuu.

Yanga, Azam fc na Coastal ni klabu zilizotumia fedha nyingi katika maandalizi ya msimu huu, japokuwa Azam walifanya hivyo kabla ya ligi kuanza.

Malengo ya Coastal na Yanga kwenda nje ya nchi kabla ya kuanza mzunguko wa pili yalikuwa ni kusaka ubingwa au nafasi tatu za juu.

Hata katika usajili, Coastal walinasa nyota kibao wakiwemo akina Haruna Moshi `Boban`, Juma Nyoso, Kato Yayo kutoka Uganda, Mkenya Crispian Odula, Jerry Santo, Shaban Hassan Kado na wengine wengi.

Mbali na kusajili nyota hao, pia kuna wachezaji wengine wenye viwango vizuri.

Akina Fikirini Suleiman, Hamadi Juma, Abdi Banda, Yusuf Chuma, Mbwana Kibacha, Razak Khalfan, Ally Nassor ‘Ufudu’, Behewa Sembwana, Suleiman Kassim ‘Selembe’, Kenneth Masumbuko, Danny Lyanga ni wachezaji wazuri sana.

Pia wapo akina Mansour Alawi, Ayoub Masoud, Marcus Ndeheli, Ayoub Semtawa, Mohammed Miraji, Crispian Odula, na Mohammed Kipanga.

Coastal Union ina wachezaji wa aina zote. Wapo wenye uzoefu na vijana wadogo.

Mechi za mwisho, kocha Chipo aliamua kutumia vijana wengi ambao walionekana kukiongezea kasi kikosi chake.

Binafsi nafasi ya tisa kwa Coastal naiona kama hukumu kubwa kwao.

Kwa jinsi walivyotumia mkwanja mrefu hawakustahili kukaa katika nafasi hiyo.

Lakini ukirudi uwanjani, jinsi wachezaji hawa wanavyocheza, utagundua kuna kitu hakiko sawa klabuni hapo.

Wachezaji wanafanya uzembe mwingi bila sababu na wanakuwa chini ya morali katika mechi nyingi.

Nadhani mivutano ya muda mrefu ya viongozi wa Coastal Union imekuwa chanzo kikubwa kwa klabu hiyo kufanya vibaya.

Hakuna uelewano wa viongozi kwenye baadhi ya mambo ya msingi.

Tulisikia juzi juzi wanachama wa Coastal wakilalamika kubaniwa kadi za uanachama kwa muda mrefu bila sababu ya msingi.

Coastal ni timu ya watu, lakini viongozi wamekuwa na mambo yao kinyume na matakwa ya mashabiki wao.

Hata maamuzi ya kumfukuza kocha Hemed Morroco yalichukuliwa kwa matakwa ya watu wachache na si kwa mafanikio ya klabu.

Mara nyingi Morroco alikuwa anakaririwa akisema haelewi kwanini wachezaji wake wanashindwa kufanya vizuri.

Nadhani ilifika wakati hakuwa na uhusiano mzuri na mabosi wake mpaka anaamua kuondoka.

Lakini ishu kubwa sio kwa viongozi kuvutana, hata wachezaji wana wajibu wa kuivusha klabu kufika pale inapohitaji.

Timu ina Boban, Nyoso, Kato, Odula, Santo inashindwaje kukaa hata timu nne za juu au hata sita basi.

Hakika wachezaji wa Coastal wanatakiwa kukaa chini na kufanya tathmini ya kuboronga kwao msimu huu.

Wamekaa kambi nzuri, wamepewa pesa na kupelekwa mpaka Oman, lakini wanaifanya klabu kuwa ya tisa.

Hakika kila mtu ndani ya Coastal Union anatakiwa kuwajibika kwa nafasi yake.

Kama kuna matatizo ya uongozi, basi wakae chini na kumaliza mivutano yao ili waifanikishe timu.

Kufanya vibaya ni kuwakatisha tamaa wadhamini wao. Nani wakuweka pesa sehemu isiyokuwa na faida?.

Mtu anapoamua kuwekeza ndani ya timu, anategemea kufanya biashara na kufikia malengo yake.

Kiukweli hakuna mtu anayeweza kuwekeza sehemu ambayo hailipi.

Coastal wanatakiwa kujipanga vizuri ili kupata mafanikio sawa na pesa wanazowekeza.

Wachezaji nao wajipange upya.  Kwa wale watakaokuwepo msimu ujao waje na mtazamo mpya wa kuisaidia timu.

Moja kati ya amri kuu ya mpira miguu katika amri zake 10, ni mchezaji kucheza kwa faida ya timu.

Kama timu inashindwa kupata matokeo, nawewe mchezaji kwa jitihada zako binafsi unaona unaweza kuiokoa, basi fanya kazi hiyo kwa maslahi ya timu.

Lakini wachezaji wa Coastal Union  kuna wakati wanaonekana kuwa chini ya kiwango na ukiwaangalia unagundua kuna tatizo vichwani mwao.

Poleni Coastal Union, huo ndio mpira, lakini jipangeni sawasawa kwa msimu ujao.

Mkienda tena Oman mje na nguvu kubwa zaidi, na sio kuwa wachovu kama ilivyotokea msimu huu.


Viongozi wa klabu kaeni chini kujua wapi mmekosea ili kuisaidia timu yenu msimu ujao.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video