Thursday, April 24, 2014



Na Baraka Mpenja, Dar es salaam
MABADILIKO ya mfululizo katika  benchi la ufundi imetajwa kuwa moja ya sababu ya Wekundu wa Msimbazi kufanya vibaya msimu wa 2013/2014 uliomalizika aprili 19 mwaka huu kwa timu hiyo kutoka sare ya bao 1-1 na watani zao wa Jadi, Yanga SC.
Simba walimaliza ligi wakiwa katika nafasi ya 4 baada ya kujikusanyia pointi 38 pekee katika michezo 26.
Ally Mayay Tembele, beki na nahodha wa zamani wa Yanga sc na sasa kocha wa mpira wa miguu amesema kuwa kubadili benchi la ufundi mara kwa mara kunaleta athari ya moja kwa moja katika kikosi.
“Kila mwalimu ana falsafa yake, kwahiyo unapobadili kocha ujue kabisa unaleta mfumo mpya katika klabu ambao utahitaji muda ili wachezaji wazoee”.
“Msimu wa 2011/2012 alikuwepo kocha Mserbia Milovan Circovic, baadaye akaja mfaransa Patric Liewig. Akiwa ameshaanza kuijenga Simba ya vijana na sasa wanaanza kumuelewa, akaondolewa na kuletwa Abdallah Kibadeni. Hawa ni walimu watatu tofauti na wana aina yao ya ufundishaji”
“Wachezaji ndani ya muda mfupi walijikuta wakilishwa mifumo tofauti. Sasa walishindwa kushika kwa haraka kwasababu wakianza kuzoea kunatokea mabadiliko”
“Kibadeni alikuwa ameanza kuwaweka vijana wake vizuri na tuliona Simba ikianza kutambulika na makinda wake, ghafla anatimuliwa na analetwa Mcroatia Dravko Logarusic; Huyu naye ana mfumo wake”.
“Kwa mazingira haya, Simba isingeweza kutengamaa kwa haraka na walihitaji muda sana”. Alisema Mayay ambaye pia ni mchambuzi wa Soka.
Simba kwasasa wapo katika mazungumzo na kocha Logarusic ili kuoana kama wanaweza kumpa mkataba mwingine.
Katibu mkuu wa Simba, Ezekiel Kamwaga alisema hatima ya kocha huyo ni mwishoni mwa wiki hii’
Kamwaga alikaririwa akisema: “Simba tunamhitaji Loga tofauti na watu wanavyodhani. Cha msinhgi ni kuwa kwasasa tuko katika mazungumzo ya mkataba mpya. Mwishoni mwa wiki hii tutaweka mambo hadharani”.
Kocha Loga amekuwa akishutumiwa na wachezaji kuwa anawabebesha mzigo mzito na ni mkali mno pale wanapohitaji busara zake.
Loga ni muumini mkubwa wa nidhanu na ana msimamo mkali kwa wachezaji na viongozi wake.
Mara nyingi amekuwa akiwaadhinu wachezaji wake uwanjani pale wanapofanya makosa.
Hauno shida kumkalisha mchezaji benchi au kumtoa dakika yoyote ya mchezo kama anafanya uzembe tofauti na matarajio yake.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video