SAFU ya ulinzi ya Barcelona imezidi kupata majanga baada ya
taarifa za mchana huu kueleza kuwa beki wake Carles Puyol aliyetarajiwa kucheza
mechi ya kesho jumapili dhidi ya Atlectic Bilbao ameumia tena.
Klabu imesema Puyol ambaye pia alitegemewa kucheza mechi ya Copa
del Rey mapema wiki hii, ataikosa mechi ya kesho baada ya kutonesha goti lake
wakati akifanya mazoezi.
Barcelona tayari inamkosa beki wake Gerard Pique na Jordi Alba
na mshambuliaji wake Neymar na mlinda mlango Victor Valdes.
Beki Marc Bartra amejumuishwa katika kikosi cha kesho baada ya
kuripotiwa kuwa katika hatari ya kukosa mechi hiyo.
Barcelona wanahitaji kushinda mehi ya kesho ili kubakiza pointi
nne nyuma ya vinara, Atletico Madrid.
0 comments:
Post a Comment