Sunday, April 20, 2014

article-2608806-1D38DC0B00000578-769_634x402
ARSENAL wameendelea kujiongezea matumaini ya kuingia timu nne bora msimu huu baada ya ushindi wa mabao 3-0 jioni hii dhidi ya wana fainali wenzao wa kombe la FA, Hull City  kwenye uwanja wa KC.
Mjerumani, Lukas Podolski  amefunga mabao mawili katika dakika ya 45 na 53, lakini Aaron Ramsey ndiye alikuwa wa kwanza kuandika  bao la kwanza katika dakika ya 31 kipindi cha kwanza, na kuwafanya Asernal wawe juu ya Everton bila kujali matokeo ya mechi inayoendelea muda huu Goodison Park kati ya Everton na Manchester United.
Hull walicheza vizuri kipindi cha kwanza, lakini bao la pili la Podolski katika dakika za mwanzo za kipindi cha pili liliwachanganya na sasa wanahitaji kujipanga zaidi kabla ya kukutana na Asernal mwezi ujao.
Baada ya ushindi wa huu, Asernal wanafikisha pointi 70 katika nafasi ya 4, wakati wapinzani wao Everton waliopo nafasi ya 5 kwa pointi 66 wapo uwanjani kuumana na Man United.
Ramsey amerejea leo baada ya kukaa nje ya uwanja wa muda mrefu kutokana na majeruhi, na urejeo wake umekuwa na faida kwa timu kwasababu amecheza mpira mzuri na kufunga bao muhimu.
Naye Mesut Ozil ambaye hajacheza tangu machi 11 ameonekana leo na kuonesha soka zuri.
Ushindi huu ni muhimu kwa kocha Asernal Wenger kwasababu ndoto zake ni kutafuta nafasi ya nne ili kushiriki ligi ya mabingwa barani Ulaya msimu ujao.
Asernal walianza ligi vizuri na kuongoza kwa muda mrefu, lakini walianza kupoteza mwelekeo na hatimaye kuwaachia Liverpool, Chelsea na Man City waendeleze vita ya ubingwa.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video