Sunday, March 9, 2014

Na Baraka Mpenja
0712461976 au 0764302956

BAHATI haikuwa kwa Yanga usiku huu. Wametolewa na Al Ahly kwa mikwaju ya penati katika mchezo wa marudiano ligi ya mabingwa barani Afrika kuwania hatua ya 16 bora baada ya kufungwa bao 1-0 ndani ya dakika 90.

Mabingwa watetezi, National Al Ahly wamepata penati 4  huku Young Africans wakipata penati 3.

Waliofunga penati za Yanga ni  Didier Kavumbagu `Kavu`, nahodaha na beki wa kati, Nadir Haroub `Canavaro`,  na Emmanuel  Anord Okwi .

Wanandinga wa Yanga waliokosa penati usiku huu ni Oscar Samwel Joshua , Said  Bahanuzi na Mbuyu Twite .

Mlinda mlango namba moja wa Yanga Deogratius Munishi ‘Dida’ alipangua penalti mbili mfululizo ya nne na ya tano, lakini Yanga SC nao wakakosa penalti mbili mfululizo ya nne na ya tano.

Mbali na kupangua penati hizo, alicheza vizuri ndani ya dakika 90 na kuwa kikwazo kikubwa kwa Al Ahly kupata ushindi.

Mchezo wa leo umemalizika kwa Yanga kufungwa bao moja sawa na matokeo waliyoyapata Yanga katika mechi ya kwanza jijini Dar es salaam, Machi mosi mwaka huu uwanja wa Taifa.

Bao la Alhly ndani ya dakika 90 lilifungwa katika dakika ya 70 na baada ya hapo liliwaamsha zaidi wenyeji hao na kuongeza mashambulizi katika lango la Yanga.

Yanga walipata nafasi za kufunga katika dakika ya 54 kipindi cha pili ambapo winga mwenye kasi kubwa, Simon Msuva alikosa umakini.

Dakika ya 89, Frank Domayo `Chumvi` aliikosesha Yanga bao la kusawazisha baada ya kushindwa kutumia nafasi aliyoipata.

Kipindi cha kwanza  Waarab walikuwa golini kwa Yanga kwa muda mwingi, huku Yanga wakifanya mashambulizi ya kushtukiza, lakini dakika 45 za kipindi cha kwanza zilimalizika bila kufungana.

Yanga walihitaji sare au suluhu, kama si hivyo kufungwa kwa toafauti ya bao moja, ,mfano, 2-1, 3-2 ili kusonga mbele ndani ya muda wa kawaida.

Kufungwa bao moja kumewalazimu kwenda hatua ya penati ambayo huwa ni bahati tu na si ufundi muda mwingine.

Matokeo ya Yanga yamewaumiza mashabiki, wanachama, viongozi, benchi la ufundi na watanzania kwa ujumla, kwani wao ndio walibaki wawakilishi pekee wa nchini katika michuano ya ligi kuu.

Kwasasa Timu zote za Tanzania zimetolewa katika mashindano ya Kimataifa.

Poleni sana wana Yanga kwa matokeo hayo, huo ndio mpira. Jipangeni upya na mrudi ligi kuu ili mtetee ubingwa wenu na kushiriki tena mwakani.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video