Thursday, March 6, 2014

YANGA TUAPicha na Saleh Jembe.com, Misri
Na Baraka Mpenja, Dar es salaam

0712461976/0764302956

MABINGWA wa ligi kuu soka Tanzania bara na wawakilishi pekee wa nchi katika michuano ya kimataifa, Dar Young Africans tayari wamewasili jijini Cairo kujiandaa na mchezo wa marudiano wa ligi ya mabingwa barani Africa utakaopigwa jumapili machi 9 mwaka huu dhidi ya mabingwa watetezi wa kombe hilo,  klabu ya National Al Ahly.

Taarifa kutoka Misri zinaeleza kuwa baada ya wachezaji, benchi la ufundi na viongozi wa klabu ya Yanga SC kufika uwanja wa ndege mjini humo, waandishi wa habari walitaka kuzungumza na wachezaji, lakini hakuna mchezaji yeyote aliyezungumza nao kwa sababu maalumu.

Waandishi hao baada ya kuchuniwa na wanajangwani, waliishia kuwapiga picha wachezaji, viongozi pamoja na basi walilopanda kuelekea Katika Hotel waliyokusudia kuweka kambi.

Waarabu wamekuwa na utamaduni wa kufanya fitina kwa timu za kigeni kila zinapokwenda kucheza kwao, lengo likiwa ni kuwaondoa mchezoni wapinzani ili wawafunge kirahisi.

Mwaka 2003, Mnyama Simba aliwatoa Zamalek na kuwavua ubingwa wakiwa kwao Cairo kwa njia ya mikwaju ya penati, lakini kabla ya mchezo huo, zilifanywa fitina nyingi sana ili kuwafunga Simba.

Simba wakiwa katika ubora wa hali ya juu ndani ya uwanja na nje ya uwanja, walikabiliana na changamoto zote, huku viongozi wakiongozwa na `Friends of Simba` walikuwa makini kusimamia kila kitu ili fitina za Zamalek zisiathiri mchezo.

Hatimaye walishinda na kuwatoa wenyeji wao, hivyo kuleta heshima kubwa kwa Tanzania.

Leo baada ya Yanga kuwasili, nao Al Ahly wanaonekana wamekusudia kufanya fitina kwani wamekuwa wakichelewesha baadhi ya mambo ya msingi kisheria ikiwemo kutowafahamisha Yanga uwanja utakao tumika jumapili.

Yanga wamejiandaa kwa lolote lile, ndio maana inawezekana wamewakataza wachezaji wao kuongea na waandishi wa habari wa Misri wanaoiunga mkono timu yao.

Wanajangwani wataingia katika mchezo huo wakiwa na faida ya ushindi wa bao 1-0 katika mchezo wa kwanza uliofanyika uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam Machi mosi mwaka huu.

Bao hilo pekee lilifungwa na beki wakati na nahodha wa klabu hiyo, Nadir Haroub `Canavaro` katika dakika ya 82 ya mchezo.

Yanga wanahitaji sare yoyote ile au suluhu, au matokeo ya kufungwa kwa tofauti ya bao moja, mfano 2-1 ili wafaidike na bao la ugenini.

Kikosi cha Mholanza Hans Van Der Pluiljm kimekuwa kikijaanda kwa takribani wiki nzima katika hoteli ya Bahari Beach kunduchi jijini Dar es salaam, hivyo kina nafasi ya kushinda endapo wachezaji watakuwa makini.

Wachezaji wa Yanga wanahitaji kuwa watulivu na kutambua kuwa kuna mashabiki wengi wapo nyuma yao, hivyo fadhila kwao ni kuucheza mpira kwa nguvu zote.

Taarifa kutoka Misri zinaeleza kuwa hali ya wachezaji ni nzuri, kiafya, fikra na morali ya kuelekea mchezo wenyewe bado ni kubwa kwani bench la ufundi na wachezaji wanaamini maandalizi wanayoyafanya yatasaidia kupelekea kupata ushindi katika mchezo huo na kuweza kusonga mbele katika hatua ya 16 bora.



Mchezo wa jumapili unatarajiwa kufanyika katika uwanja wa Arab Contractors uliopo jijini Cairo huku mechi hiyo ikichezwa bila ya mashabiki kufuatia Serikali ya Misri kuzuia mashabiki wa soka kutokana na mashabiki hao kufanya vurugu katika mchezo wa Fainal ya Super Cup dhidi ya CS Sfaxien na kupelekea askari kadhaa kujeruhiwa.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video