Friday, March 7, 2014

Uwanja wa Border Guard utakaotumiwa kwa mchezo wa Yanga na Al Ahly Jumapili

Na Baraka Mpenja , Dar es salaam


0712461976 au 0764302956
HATIMAYE  Al Ahly wametaja uwanja utakaotumika katika mchezo wa marudiano  ligi ya mabingwa barani Afrika dhidi ya mabingwa wa ligi kuu soka Tanzania bara na wawakilishi pekee wa Tanzania kwenye mashindano ya kimataifa, Dar Young Africans.

Shirikisho la soka nchini Misri limesema kuwa mchezo huo wa jumapili machi 9 mwaka huu  utafanyika mjini Alexandria katika Uwanja wa Border Guard stadium (Haras el Hadod) .

Awali mchezo huo  ulitakiwa kufanyika  mjini Cairo na sasa utafanyika katika mji wa Alexandria takribani kilometa zaidi ya 200 kutoka Cairo ambapo kikosi cha Young Africans kimeweka kambi kujiandaa na mchezo huo.

Taarifa kutoka kwa viongozi wa Yanga wakiongozwa na makamu mwenyekiti wake C iment Sanga imeleza kuwa baada ya kupewa taarifa kupitia Ubalozi wa Tanzania nchini Misri, tayari wameanza maandalizi ya kuhakikisha timu inakwenda mjini Alexandria kucheza mchezo huo wa jumapili na kufanya vizuri.

Hata hivyo Yanga wameshangazwa na taarifa za Uwanja  kutolewa siku tatu kabla ya mchezo huku wahusika wakitambua kuwa Young Africans ilifahamu mchezo huo utafanyika Cairo takribani wiki mbili zilizopita na viongozi wa Al Ahly waliopokuwa nchini Tanzania walidhibitisha hilo.

Sehemu ya taarifa hiyo imesema kuwa  “Pamoja na mabadiliko hayo ya ghafla ya sehemu utakapofanyika mchezo siku ya jumapili, benchi la ufundi pamoja na wachezaji na viongozi waliopo jijini Cairo bado wana imani ya kufanya vizuri na kusonga mbele katika hatua ya 16 bora”.

Wakati hayo yakijiri, nao washambuliaji wa Yanga raia wa Uganda, Hamisi Kizza na Emmanuel Okwi tayari wameshawasili jijini Cairo usiku wa jana majira ya saa 7 kwa shirika la ndege la Egypt Air wakitokea nchini Zambia walipokuwa wakiiwakilisha timu yao ya Taifa kwenye mchezo wa kirafiki siku ya jumatano dhidi ya Zambia na The Cranes kulala kwa mabao 2-1.

Katika mchezo huo uliopigwa mjini Lusaka, bao la Uganda lilifungwa na Hamis Friday Kiiza na .

Mchezo huo wa siku ya jumapili ambao unafanyika mjini Alexandria katika Uwanja wa Border Guard Stadium (Haras El Hadod) hautakua na watazamaji kutokana na mamalaka ya ulinzi na usalama kuzuia mashabiki kuingia katika mchezo wowote wa mpira wa miguu nchini Misri. 

Yanga wataingia uwanjani wakiwa na faida ya ushindi wa bao 1-0 walioupata katika mchezo wa machi mosi , uwanja wa Taifa jini Dar es salaam.

Bao pekee la Yanga lilifungwa katika dakika ya 82 na beki wa kati na nahodha wake,Nadir Haroub `C

Canavaro` kwa njia ya kichwa.

Inafahamika kuwa Waarabu wana fitina sana wanapokuwa nyumbani kwao, lakini umoja wa Yanga na kujituma kwa wachezaji wao ndio itakuwa silaha pekee ya kuwaangusha wenyeji wao.

Yanga wanahitaji sare au suluhu katika mchezo huo, au kama wanafungwa basi wafungwe kwa tofauti ya bao moja mfano; 2-1, 3-2 ili wanufaike ba bao la ugenini.

Al Ahly wataingia uwanjani kwa lengo la kutafuta mabao zaidi, lakini Yanga watatakiwa kuwa makini muda wote wa mchezo hasa dakika za kwanza ili wasifungwe mapema na kuvurugwa zaidi.

Kila mchezaji wa Yanga anatakiwa kufahamu kuwa watanzania wapo nyuma yao wakiwaombea dua, cha msingi wafanye kazi yao kwa bidii ili kubadili historia ya udhaifu wa Yanga kwa timu za kaskazini mwa Afrika.

Mtandao huu unawatakia kila la heri Yanga katika mchezo huo mkubwa wa jumapili.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video