Monday, March 10, 2014

 Na Baraka Mpenja , Dar es salaam
0712461976 au 0764302956

WALIOKUWA wawakilishib pekee wa Tanzani  michuano ya Kimataifa, Young Africans SC wametolewa kwenye mashindano ya Klabu Bingwa Barani Afrika na mabingwa watetezi Al Ahly kwa mikwaju ya penati 4-3 usiku wa jana katika Uwanja wa El Max jijini Alexandria

Mshindi wa mchezo huo alilazimika kupatikana kwa mikwaju ya penati kufuatia kumalizika kwa dakika 90 za mchezo huo huku  Al Ahly  wakiwa mbele kwa bao 1-0 sawa na matokeo ya Dar es salaam , hivyo kufanya matokeo ya jumla kuwa 1-1.

Licha ya kupoteza mchezo huo, Yanga walipigana kiume kutoka mwanzo hadi mwisho wa mchezo.

Yanga walionekana kucheza kwa kujituma zaidi kwani walitambua wazi kuwa Watanzania wengi hasa mashabiki wao wapo nyuma yao.

Haikuwa rahisi kwa Yanga kupata ushindi katika mchezo wa jana kutokana na ukweli kuwa waarabu wanacheza  mpira mkubwa sana wakiwa nyumbani kwao.

Al Ahly katika mechi ya kwanza Uwanja wa Taifa , jijini Dar es salaam walicheza mpira wa taratibu zaidi, huku nusu yao wakiwa nyuma kulinda lango lao.

Yanga walishambulia sana lango wa Al Ahly, lakini waarabu walikuwa makini.

Kwa upande mwingine washambuliaji wa Yanga walishindwa kutumia nafasi walizopata.

Katika mchezo wa jana, Al Ahly si wale waliocheza Dar es salaam. Kwa haraka mtu anaweza kugoma kabisa. Walikuwa na kasi kubwa na mashambulizi mengi zaidi.

Walifahamu kabisa kuwa wanahitaji ushindi katika mchezo huo, hivyo waliingia kwa kazi ya kutafuta mabao.

Wakati waarabu wakihaha kutafuta mabao katika mchezo huo uliochezwa bila mashabiki kuwepo uwanjani, Yanga walionesha utulivu mkubwa katika safu ya ulinzi ikiongozwa na nahodha, Nadir Haroub `Canavaro`.

Kipindi kizima cha kwanza, Al Ahly walishindwa kufurukuta na kutikisa nyavu za Yanga.

Kwa upande wa Yanga wao waliingia uwanjani wakiwa makini na kufanya mashambulizi kadhaa langoni mwa lango la Al Ahly.

Kikwazo kilikuwa kwa wachezaji wa Yanga, Didier Kavumbagu , Simon Msuva na Frank Domayo ambao walikosa umakini katika nafasi za wazi walizopata.

Bao la dakika ya 70 walilopata Al Ahly kupitia kwa beki wao wa kushoto Al Ahly Saed Mowaeb liliwaamsha zaidi na kuwashambulia Yanga kwa nguvu.

Mchezo ukawa mgumu zaidi kwa wanajangwani, lakini walinzi wake Kelvin Yondani, Nadir Haroub walikua makini kuokoa michomo hiyo huku mlinda mlango Deogratius Munishi `Dida` akifanya kazi ya ziada kuokoa hatari langongi mwake.

Kipindi hicho cha pili hakikuwa kizuri sana kwa Yanga,  japokuwa walifanya mashambulizi kadhaa langoni mwa wapinzani wao, lakini mwamuzi wa mchezo huo kutoka nchini Senegal aliwaonesha kadi za njano wachezaji wa Yanga na kupuliza filimbi kila wachezaji wa Al Ahly walipoguswa kawaida tu.

Sitaki kuamini kuwa alikuwa akiwapendelea wenyeji, lakini kuna wakati alikuwa akizidisha mno. Wachezaji wa Al Ahly walikuwa wakiguswa kawaida .

Hizo ni mbinu katika mpira wa miguu, cha msingi unapogundua wapinzani wako wanasaidiwa na mwamuzi kila wanapoguswa na kujiangusha, unatakiwa kuongeza umakini.

Na ndivyo ilivyokuwa kwa Yanga. Walionesha ukomavu na uvumilivu mkubwa hapo jana.


Baada ya dakika 90 kumalizika kwa Yanga kufungwa bao 1-0, mwamuzi aliamuru zipigwe penati.

Mikwaju ya penati kuna wakati inafungwa kwa ufundi, lakini kuna muda unaweza kuamini katika bahati.

Tumeshuhudia wanasoka maarufu kama Ronaldo na Messi na wengine wengi wakikosa penati katika michezo mbalimbali.

Kukosa penati sio kesi. Kuna wakati inakuwa ni bahati tu.

Yanga walipata penati 3 huku wenyeji wao wakipata 4.

Waliofunga penati za Yanga ni Nadir Haroub , Didier Kavumbagu, na Emmanuel Okwi

Wakati huo penati ya Oscar Joshua iligonga mwamba , Said Bahanuzi   ilitoka nje, na ya Mbuyu Twite  iliokolewa na golikipa Ekramy.

Al Ahly penati zao zilifungwa na Abdalllah Said, Gedo, Trezeguet na Mohamed Nagieb,  huku mlinda mlango Deo Munshi akipangua penati mbili za Saed Mowaeb na Hossan Ashour

Nawapongeza Yanga kwa kucheza kwa kujituma ingawa malengo yao hayakutimia.

Kinachotakiwa si kukata tamaa, wajiandae kwa wakati mwingine kwani wanacho kikosi bora cha kushindana.

Najua watabezwa sana na mashabiki wa upande wa pili pamoja na viongozi, lakini wanatakiwa kutambua kuwa utani katika mpira una nafasi yake.

Warudi nyumbani na kuelekeza nguvu zao ligi kuu soka Tanzania bara ili kutetea ubingwa wao.

Wapo nafasi ya tatu katika msimamo, lakini wanayo michezo mkononi, cha msingi ni kusahau matokeo ya jana na kuanza upya kazi ya kuutafuta ubingwa wa ligi kuu.

Kama watatwaa ubingwa msimu huu watapata nafasi nyingine ya kushiriki katika michuano hiyo mikubwa barani Afrika kwa ngazi ya klabu.

Kwa kiwango cha Yanga katika mchezo wa jana ambao ulikuwa mgumu namna kwao,  unaweza kugundua kirahisi kuwa Yanga wamejiamini na wana kikosi bora msimu huu.

Bila shaka waarabu wamelala na viatu huku mashabiki wao wakishangilia usiku kucha mitaani jijini Cairo, kwani ushindi wao ulipatikana kwa nguvu sana.

Yanga walikuwa wanawashinda Al Ahly katika maarifa ya kufumania nyavu, na endapo vijana wa Hans Van Der Pluijm wangekuwa makini wangefunga mabao.


Poleni wana Yanga wote, huo ndio mpira. Njooni nyumbani mcheze ligi kuu. 

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video