Tuesday, March 4, 2014

MMG25849Na Baraka Mpenja, Dar es salaam

Tel: 0712461976 au 0764302956


MABINGWA wa soka Tanzania bara na wawakilishi pekee wa nchi katika mashindano ya kimataifa, klabu ya Yanga ya Dar es  salaam imeanza kujifua jana kuelekea katika mechi ya marudiano dhidi ya mabingwa watetezi wa ligi ya mabingwa barani Afrika, klabu ya National Al Ahly ya Misri itakayopigwa mjini Cairo jumapili machi 9 mwaka huu.


Yanga wataingia uwanjani wakiwa na mtaji wa ushindi wa bao 1-0 walioupata katika mchezo wa awali,  uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam machi mosi mwaka huu.


Bao hilo pekee lilifungwa dakika ya 82 kupitia kwa nahodha na beki wake wa kati Nadir Haroub `Canavaro`.


Kuelekea katika mchezo huo, kiungo wa zamani na nahodha wa Yanga, Ali Mayay Tembele amewashauri wana Jangwani kujiandaa vizuri kwani Waarabu wataingia kwa nguvu kubwa kuhitaji kufuta matokeo ya mchezo wa awali.


Mayay alisema Al Ahly wakicheza jijini Dar es salaam walikuwa wakicheza mpira wa taratibu, huku wakitumia mbinu za kupoteza muda kwa lengo la kulazimisha sare ugenini wakitarajia kumaliza kazi mjini Cairo.


“Waarabu wamekuwa na utamaduni wa kuhitaji sare au ushindi ugenini. Huwa wanacheza mpira wa kawaida, lakini wakirudi kwao wanakuja na aina nyingine ya mpira ambao huwa unawatimizia malengo yao. Kikubwa Yanga wanatakiwa kujiandaa ipasavyo na kufuta makosa yao ya mchezo wa awali”. Alisema Mayay.


Mchambuzi huyo na kocha wa mpira wa miguu kwa sasa aliongeza kuwa Yanga walipoteza nafasi za kupata mabao mengi nyumbani, lakini ushindi ni ushindi tu.


“Kwenye mpira tunasema ushindi ni ushindi tu. Bao moja walilopata Yanga ni muhimu kwao, huwezi jua nini kitatokea Cairo, lakini lazima jitihada za pekee zitatumika kulilinda bao hilo.”. Alisema Mayay.


Aidha alisisitiza kuwa Yanga ina wachezaji wenye uwezo wa kuwapatia matokeo mazuri wakiwa ugenini, hivyo ni jukumu la benchi la ufundi kurekebisha makosa yao na kuwatumia kiusahihi.


“Timu ina Okwi, Kiiza, Ngassa na Msuva kule mbele. Katikati wapo Domayo, Niyonzima, Chuji. Nyuma wapo Yondan, Canavaro, Twite, Joshua, Luhende. Ukiangalia uwezo wa mchezaji mmoja mmoja utagundua kuwa Yanga wana watu wa kuwasaidia endapo watakuwa makini kwenye mchezo wao na kutumia kila nafasi watakayobahatika kupata”. Alisema Yanga.


Mayay aliongeza kuwa tofauti ya timu kubwa na ndogo ilionekana uwanja wa Taifa kwani Yanga walipata nafasi nyingi na kuzipoteza, lakini endapo Waarabu watapata nafasi kama zile itakuwa ngumu sana kuzipoteza.


“Binafsi naelewa kuwa Al Ahly watacheza soka la kushambulia sana. Kitakachohitajika kwa Yanga si kucheza kwa kujihami. Watatakiwa kucheza mpira wa kwenda mbele ili angalau kupata bao na kuwachanganya wenyeji wao”. Alisema Mayay.


Kufuatia matokeo ya 1-0 uwanja wa Taifa, Yanga SC sasa inahitaji sare ya ugenini au kufungwa kwa tofauti ya bao moja ili wasonge mbele hatua ya 16 Bora kwa faida ya bao la ugenini.


Kihistoria hii imekuwa mara ya kwanza kabisa  kwa Yanga SC kupata ushindi dhidi ya timu ya Misri na Kaskazini mwa Afrika kwa ujumla, kwani mara zote imekuwa ikifungwa na kutoa sare.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video