Monday, March 3, 2014

SIMBASC2Vijana wa Logarusic wana kibarua kizito machi 9 jijini Mbeya dhidi ya Tanzania Prisons. Na tayari wameshapigwa Mkwara mzito wa kurejea na maumivu ya kufungwa.
TFF-Tanzania-PrisonsHawa nao safari hii ni hatari tupu, wamekuja juu sana
Na Baraka Mpenja ,  Dar es salaam
Tel: 0712461976 au 0764302956
WAJELAJELA Tanzania Prisons wametamba kuibamiza Simba Sc ya jijini Dar es salaam katika mchezo wao wa ligi kuu soka Tanzania bara jumapili ya machi 9 mwaka huu uwanja wa Sokoine jijini Mbeya.
Akizungumza kwa kujiamini na mtandao huu, katibu mkuu wa klabu hiyo Inspekta Sadick Jumbe, amesema mnyama hana ubavu wa kutoka katika mchezo huo kutokana na kuimarika kwa kikosi chao mzunguko huu wa pili wa ligi kuu.
“Lazima ufahamu kuwa kikosi chetu chini ya kocha wetu David Mwamwaja kimeimarika sana. Mpaka sasa hatujapoteza mechi hata moja. Jana Mgambo wametubana mbavu na kutoka nao sare ya 1-1, lakini nakuhakikishia, tuna hamu na mnyama jumapili na hataweza kutoka”. Alisema Jumbe.
Jumbe aliongeza kuwa ushindi wa jana walioupata Simba wa mabao 3-2 dhidi ya wajeruhiwa Ruvu Shooting uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam , umewaongezea nguvu zaidi, lakini watahakikisha wanawarejesha katika machungu kwa mara nyingine zaidi.
“Vijana wapo katika morali kubwa, wanafahamu kuwa timu inatakiwa kujinusuru kushuka daraja, na ndio maana ukiwaona kwa kila mchezo wanajituma sana.” Alisisitiza Jumbe.

Katibu huyo amewaondoa hofu mashabiki wa soka wa Mbeya ambao wana wasiwasi na klabu yao kushuka daraja, kwani walishagundua makosa yao na kuyafanyia kazi ikiwa ni pamoja na kubadili benchi la ufundi.

“Tunafurahishwa sana na sapoti kubwa ya mashabiki mzunguko huu wa pili, wameonesha uzalendo mkubwa, tunaheshimu sana mchango wao na sisi tuko imara kuwafanya wafurahi zaidi. Hatushuki daraja nakwambia ”. Aliongeza Jumbe.

Kwa upande wao Simba kupitia kwa Afisa habari wao, Asha Muhaji wamesema kila wanapocheza mechi na kukamilisha dakika 90, wanasahau na kuangalia ya mbele.

‘Ligi ni ngumu sana, matokeo si rahisi kutabiri. Unaweza kuamini kuwa unaifunga timu fulani, lakini mambo yakawa tofauti. Simba tunaendelea kujiwinda na mechi zilizosalia kuhakikisha tunapata matokeo mazuri”. Alisema Asha.

Aidha Asha aliwaomba mashabiki wao kuwa na subira kwani timu yao ni nzuri, na matokeo yanayopatikana kwa siku za karibuni ni sehemu ya mpira.
“Yanazungumzwa mengi kuhusu Simba, kila mtu analeta yakwake. Tusiwe wepesi wa kukubali maneno ya mitaani yaharibu timu yetu. Mashabiki watambue timu ni yao na wanatakiwa kuendelea kujitokeza uwanjani kuisapoti Simba yetu”. Alisema Asha.

Simba katika mechi sita ilizocheza mzunguko huu wa pili imefungwa mechi mbili, kutoka sare mbili na kushinda mbili.

Ilishinda mabao 4-0 dhidi ya Rhino Rangers ya Tabora,  uwanja wa Taifa, Ikatoka sare ya 1-1 na Mtibwa Sugar, uwanja wa Jamhuri, ikafungwa 1-0 na Mgambo JKT Dimba la CCM Mkwakwani Tanga, ikasafiri mpaka Mbeya na kutoka sare ya 1-1 na Mbeya City.

Baada ya Mbeya ikarejea Dar es salaam uwanja wa Taifa na kufungwa mabao 3-2 na JKT Ruvu, hatimaye jana ikafanikiwa kupata ushindi wa pili dhidi ya Ruvu Shooting baada ya kuilaza mabao 3-2, huku mshambuliaji wake hatari, Amiss Tambwe akifikisha mabao 19 baada ya kufunga mawili jana kipindi cha kwanza.

Mechi ya machi 9 uwanja wa Sokoine inasubiriwa kwa hamu kubwa na mashabiki wa soka mkoani Mbeya ambao msimu huu itakuwa ni mara ya pili kwao kuiona Simba ikishuka katika dimba lao.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video