Tuesday, March 11, 2014

MIWA.MIWANa Lorietha Laurence-maelezo
Mpango wa Kurasimisha Rasilimali na Biashara za Wanyonge  Tanzania, mapema mwaka huu umeanzisha  mradi wa urasimishaji wa  mashamba ya wakulima wadogo wa zao la miwa wilaya za Kilombero na Kilosa mkoani Morogoro.
 
Aidha taarifa  ilieleza kuwa Mpango huo  utahusisha vijiji vinne vya Ruhembe, Kidogobasi,Kihelezo, Kitete-Msindazi na vingine  sita  kutoka  Wilaya ya Kilombero  Mkula ,msolwa ujamaa, Katurukila, Sonjo, Sole na Magombera.
 
Katika taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari leo jijini Dar es Salaam Jumla ya hati miliki 8,902 za kimila zimeandaliwa   3,679 zimesajiliwa na nyingine 2142 zimetolewa kwa wamiliki wa wilaya za Njombe, Mufindi na Rungwe katika kutekeleza zoezi hilo la urasimishaji lilioanza Novemba  2011.
 
Utekelezaji  huo ni wa awamu ya nne unaofanywa na MKURUBITA  kwa lengo la  kukuza  mtaji  na utawala  bora  ili kuwawezesha  wananchi kuinua mapato yao  kwa  kupunguza umaskini   kwa manufaa yao.
 
Pia MKURABITA kwa kushirikiana na wadau wake imetoa wito kwa wakulima wa   miwa  Kilosa na Kilombero  kuonana na uongozi wa vyama vya wakulima wa miwa kutoka Ruhembe, Kidatu na Msolwa kwa ajili ya  kuthibitisha umiliki  wa mashamba.
 
 MKURABITA    imeandaa mafunzo  kwa ajili ya mipango  na michanganuo ya  biashara  kwa kuwaunganisha  wakulima na Taasisi za mitaji na mikopo , baada ya kukamiliksha zoezi la mchakato wa urasimishaji wilayani Kilosa  na Kilombero.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video