Tuesday, March 11, 2014


Na Baraka Mpenja , Dar es salaam

0712461976 au 0764302956

WAGONGA nyundo wa Mbeya, klabu ya Mbeya City wanaendelea kujinoa makali yao kuelekea mchezo ujao machi 16 dhidi ya Maafande wa Jeshi la  kujenga Taifa, JKT Ruvu katika dimba la Chamazi, nje kidogo ya jiji la Dar es salaam.

Afisa habari wa klabu hiyo, Freddy Jackson amesema wachezaji wapo wapo katika hali nzuri na uimara mkubwa wa kufanya vizuri mechi ijayo.

“Maandalizi yetu ni mazuri sana na tunaendelea kujiandaa vyema ili kuhakikisha kuwa tunaibuka na pointi tatu muhimu katika mchezo huo ambazo zitatuweka katika nafasi nzuri zaidi kwenye msimamo wa ligi kuu Tanzania bara”. Alisema Freddy.

Afisa habari huyo aliwaomba mashabiki wao popote pale walipo na watanzania kwa ujumla kuendelee kuwaamini kwani wanao uwezo mkubwa wa kufanya vizuri zaidi.

Akizungumzia wachezaji wawili, Richard Peter na Mwagane Yeya waliopata majeruhi katika mchezo uliopita, Freddy alisema  Peter hataweza kucheza mechi ijayo kwani hali yake bado haijaimarika.


“Nikianzanza na hali ya mchezaji Richard Peter aliyeumia katika mchezo kati yetu na Rhino Rangers ya Tabora, mchezaji huyo hali yake bado haijatengemaa atakuwa nje kwa wiki tatu zaidi chini ya uangalizi mkubwa wa daktari wetu hivyo basi atakosa mechi ijayo . kwa ujumla mchezaji huyu bado ana maumivu ya mbavu kutokana na kuumizwa vibaya katika mechi iliyopita”. Ilisema taarifa ya Fredy.

Endeleeni kuwaamini vijana wenu
Aidha Fredy aliongezaq kuwa mchezaji mwingine Mwagane Yeya kwa sasa anaendelea vizuri baada ya kuumizwa pia na mlinda mlango wa Rihno siku hiyo hiyo.

“ Kutokana na hali yake inavyoendelea kuimarika mchezaji huyu atatumika katika mechi ijayo na Ruvu JKT”. Alisema Freddy.


Mbeya City wapo nafasi ya pili katika msimamo wa ligi kuu soka Tanzania bara wakiwa na pointi 39 nyuma ya Azam fc wenye pointi 40 kileleni.

Nafasi ya tatu inashikiliwa na Yanga wenye pointi 38 lakini wamezidiwa michezo na klabu za juu.

Nafasi ya nne wapo Simba wenye pointi 36 kibindoni.

Wakati huo huo kocha msaidizi wa Mbeya City FC Maka Mwalwisyi alisema sasa wameanza ligi upya baada ya kufungwa na Yanga.

“Jinamizi la matokeo dhidi ya Yanga liliwasumbua sana wachezaji wetu. Waliathirika sana kisaikolojia na ndio maana wakafungwa tena na Coastal Union kule Tanga. Lakini sasa tumejipanga upya na wimbi la ushindi lipo palepale”. Alisema Maka.

Aidha kocha huyo aliwataka mashabiki kuwa na subira kwani Mbeya City  FC ni klabu yenye malengo makubwa zaidi.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video