Sunday, March 30, 2014

02 (1)Mwenyekiti Mtendaji wa Tume ya kudhibiti ukimwi nchini (TACAIDS) Dkt. Fatuma Mrisho akifungua semina ya mahakimu na maofisa wa polisi kutoka mikoa ya Dae es Salaam, Pwani na Morogoro pamoja wanasheria wa serikali iliyoandaliwa na tasisi hiyo kwa watendaji wa Serikali hivi karibuni katika ukumbi wa mikutano (Serengeti) jijini Dar es salaam.
15Baadhi ya washiriki wa semina wakimsikiliza Mwenyekiti Mtendaji wa Tume ya kudhibiti ukimwi nchini (TACAIDS) Dkt. Fatuma Mrisho wakati akifungua semina ya mahakimu, maofisa wa polisi kutoka mikoa ya Dae es Salaam, Pwani na Morogoro pamoja wanasheria wa serikali iliyoandaliwa na tasisi hiyo kwa watendaji wa Serikali hivi karibuni katika ukumbi wa mikutano (Serengeti) jijini Dar es salaam.
(Picha zote na Eleuteri Mangi- MAELEZO)
……………………………………………………..
Na Eleuteri Mangi- MAELEZO
Maambukizi ya virusi vya ukimwi (VVU) yanazidi kupungua mwaka hadi mwaka Tanzania kitu ambacho kinaipa faraja ya tasisi ya Serikali inayosimamia masuala ya HIV/AIDS nchini.
Kauli hiyo ilitolewa na Mwenyekiti Mtendaji wa Tume ya kudhibiti ukimwi nchini Dkt. Fatuma Mrisho alipokuwa akifungua semina iliyoandaliwa na tasisi hiyo kwa watendaji wa Serikali hivi karibuni katika ukumbi wa mikutano (Serengeti) jijini Dar es salaam.
Washiriki wa semina hiyo walikuwa ni mahakimu, maofisa wa polisi kutoka mikoa ya Dae es Salaam, Pwani na Morogoro pamoja wanasheria wa serikali. 
Semina hiyo ililenga kuwajengea uwezo watendaji wakuu wanaosimamia na kutekeleza sheria ya ukimwi ya 2008 katika kutimiza majukumu yao ya kila siku kwa kufuata sheri, kanuni na taratibu kwa wanaohitaji msaada wa kisheria.
Dkt. Mrisho alisema takwimu zinaonesha kuwa kwa ujumla maambukuzi ya ukimwi yamepungua kwa kiasi kikubwa nchini ambapo zinaonesha kuwa Tanzania Bara na Visiwani  kuanzia mwaka 2003 hadi 2004 yalikuwa ni asilimia 7.
Mwaka 2007 hadi 2008 maambukizi yalishuka mpaka kufikia asilimia 5.7 na mwaka 2011 hadi 2012 kiwango hicho kilipungua zaidi na kufikia asilimia 5.1 ambacho ni kiwango cha kitaifa, wakati Tanzani Bara pekee kiwango cha maambukizi ya VVU  ni asilimia 5.3 zaidi ya kiwango cha kitaifa.
Taswira hii ya kupungua kwa maambukizi ya VVU ni tumaini jema kwa nchi inayolenga kufikia uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025 kwani nguvu kazi inaonekana kuendelea kuimarika na inawezekana kujenga uchumi imara kwa maendeleo endelevu.
“Kila mtu kwa namna moja au nyingine anaguswa na ugonjwa wa ukimwi maana hakuna ukoo, kijiji, wilaya na mkoa usio na mtu anayeishi na VVU na hivyo hadi nchi nzima inaguswa na hali hiyo” alisema Dkt. Mrisho.
Kwa kuzingatia hali hiyo, Dkt. Mrisho amewaasa washiriki hao wa semina na wananchi kwa ujumla kuwa VVU kwa asilimia 80 huambukizwa kwa njia ya ngono, hivyo waache ngono zembe zembe na kusimamia maadili ya kazi yao na ya kijamii ili maambukizi ya ukimwi yaweze kupungua na kufikia kiwango cha asilimia sifuri hadi kufikia mwaka 2015 ambayo ni nia na lengo la TACAIDS na Serikali kwa ujumla.
Naye Mkuu wa Kitengo cha Sheria TACAIDS Elizabeth Kaganda alisema kuwa watu wanaoishi na VVU ni binadamu kama binadamu wengine  ni lazima waheshimiwe wapate mahitaji yao ya kila siku na tiba, mwathirika naye anapaswa kumlinda mtu mwingine asipate ugonjwa wa ukimwi.
Kwa upande wake Jaji Mstaafu kutoka nchini Kenya Violet Mavisi alisema kuwa ni wajibu wa mtu mmoja mmoja  kama raia, vyombo vya dola na serikali kwa ujumla kujali haki za binadamu, kuzisimamia na kuzitekeleza kulingana na sheria za nchi ikiwemo haki ya kuishi, kumiliki ardhi, kuoa, kolewa na kuwa na familia na haki nyinginezo zinazotambulika kikatiba ndani ya nchi husika.
Jaji huyo Mstaafu Kavisi alisisitiza kuwa haki zote anazotakiwa kuzipata mtu mwingine kwenye jamii usika, ni haki hizo hizo anatakiwa kupata mtu anayeishi na virusi vya ukimwi.
Mpaka sasa Tanzania kwa hali ya maambukizi ya ukimwi mikoa inayoongoza kwa watu wanaoishi na kuishi na VVU nchini ni 10 ikiongozwa na Njombe, Iringa, Mbeya, Shinyanga, Ruvuma, Dar es Salaam, Rukwa, Pwani, Katavi na Tabora.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video