Thursday, March 6, 2014


Kaseba 
Bondia Japhet Kaseba ameahidiwa gari endapo atamzimisha bondia Thomas Mashali katika pambano lao la machi 29, ukumbi wa PTA Sabasaba jijini Dar es salaam. Bondia huyo amesema maandalizi yake yanakwenda barabara.

Na Baraka Mpenja , Dar es salaam
0712461976 au 0764302956
HOMA ya pambano la masumbwi baina ya Japhet Kaseba dhidi ya Thomas Mashali litakalofanyika machi 29 katika ukumbi wa PTA sabasaba jijini Dar es salaam kuwania ubingwa wa UBO Afrika Kilo 79 inazidi kupanda , huku maandalizi yakienda vizuri kwa mabondia hao pamoja na mabondia wengine watakaopigana siku hiyo kutoka mkoani Tanga.
Katibu mkuu wa shirikisho la ngumi Tanzania PST, Antony Luta ameuambia mtandao huu kuwa hamasa imekuwa kubwa kwa mabondia  baada ya wadau wa mchezo huo kuwaahidi zawadi baadhi yao endapo watapata ushindi.
“Siku mbili tatu hivi, tumepata hasama sana baada ya msanii wa zamani wa maigizo, Doti Nata Poshi ambaye amejitokeza na kumuahidi Kaseba gari endapo atampiga. Zawadi hii amemuahidi Kaseba tu, kama atapigwa basi ataondoka na gari yake. Hii ni hamasa kubwa sana”. Alisema Luta.
Thomas Mashali atakuwa na kibaru kizoto cha kumuonesha umwamba Japhet Kaseba
Luta alisema kaseba kuahidiwa gari itakuwa chachu kubwa kwake kutafuta ushindi kwa nguvu zote, hivyo pambana litakuwa kali sana na mashabiki wajitokeze kwa wingi siku hiyo.
Katibu huyo  aliongeza kuwa nao mabondia wa Tanga wameahidiwa pikipiki maarufu kwa jina la Bodaboda kama wataibuka na ushindi katika mapambano yao.
“Kiukweli wanapojitokeza watu kama hawa kutoa zawadi kwa mabondia, sisi watu wa masumbwi tunajisikia furaha sana. Kwa siku nyingi sana tumeachwa kama yatima”. Alisema Luta.
Luta aliwataja mabondia wa Tanga kuwa ni Alan kamoti atakayepambana na Fadhil Ally wa Dar es salaam ubingwa wa UBO raundi 10.
Mwingine kutoka Tanga waja leo waondoka leo ni J.J Ngotoka atakayepanda ulingo dhidi ya  Fredy Sayuni wa Dar es salaam ubingwa wa UBO raundi 8.
Wengine ni Aji Juma atakayeoneshana kazi na Juma Fundi pambano la raundi 8.
Naye Shaban Dunga atapanda ulingoni kutunishana msuli na  Joki Hamis.
Luta aliwaomba wadau na wadhamini wa michezo kujitokeza katika mchezo wa masumbwi kwani ni mchezo unaoweza kuliletea sifa taifa la Tanzania.
“Mchezo wa masumbwi ni mchezo wa siku nyingi, lakini wadhamini wametutupa mbali sana na inaonekana kama hauna maana. Cha msingi tunawaomba waje kwa wingi ili tuweze kufanikisha malengo yetu”. Alisema Luta.
Wakati hayo yakiendelea, bondia Japhet Kaseba amesema maandalizi yake yanakwenda vizuri huku akiwaahidi mashabiki wake ushindi.
“Binafsi namheshimu sana Mashali, lakini kutokana na maandalizi yangu nitafanya vizuri na namuomba mungu anisaidie”. Alisema Kaseba.
Simu ya Mashali haijapatikana mpaka tunaingia mtamboni, lakini tutamtafuta kujua anaendeleaje na mazoezi.


0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video