Tuesday, January 14, 2014



http://www.24tanzania.com/wp-content/uploads/2013/06/cd23Twiga-Stars.jpg
Kocha Mkuu wa Twiga Stars, Rogasian Kaijage ametaja kikosi cha wachezaji 30 wanaoingia kambini kesho (Januari 15 mwaka huu) jijini Dar es Salaam kujiandaa kwa mechi dhidi ya Zambia mwezi ujao.

Mechi hiyo ya kwanza ya mchujo kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Afrika kwa Wanawake (AWC) zitakazofanyika baadaye mwaka huu jijini Windhoek, Namibia itafanyika jijini Lusaka.

Wachezaji walioitwa kwenye kikosi hicho ni Amina Ally (Lord Baden Sekondari), Amisa Athuman (Marsh Academy), Anastazia Anthony (Lord Baden Sekondari), Asha Rashid (Mburahati Queens), Aziza Mwadini (Zanzibar) na Belina Julius (Lord Baden Sekondari).

Donisia Daniel (Lord Baden Sekondari), Esther Chabruma (Sayari Queens), Evelyn Sekikubo (Kwimba Chuoni), Fatuma Bushiri (Simba Queens), Fatuma Hassan (Mburahati Queens), Fatuma Issa (Evergreen) na Fatuma Mustapha (Sayari Queens).

Fatuma Omari (Sayari Queens), Happiness Hezron (Copa Coca-Cola Ilala), Maimuna Hamisi (U20 Tanzanite), Maimuna Said (JKT), Mwajuma Abdallah (Real Tanzanite), Mwapewa Mtumwa (Sayari Queens), Najiat Abbas (Makongo Sekondari) na Neema Paul (U20 Tanzanite).

Pulkeria Charaji (Sayari Queens), Semeni Abeid (Real Tanzanite), Shelder Boniface (Makongo Sekondari), Sophia Mwasikili (Sayari Queens), Theresa Yona (TSC Academy), Vumilia Maarifa (Evergreen) na Zena Khamis (Mburahati Queens).

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video