Mkurugenzi
Mkuu wa Mfuko wa Akiba ya Wafanyakazi Serikalini (GEPF) Bwana Daud
Msangi akizungumza na viongozi wa Serikali ya Mkoa wa Rukwa
alipotembelea Ofisi ya Mkuu wa Mkoa huo Injinia Stella Manyanya kwa
lengo la kuutambulisha mfuko huo na faida zake. Mfuko huo una fursa
mbili za kujiunga ambazo ni kwa njia ya lazima kama ilivyo kwa mifuko
mingine ya hifadhi ya jamii kwa watumishi wa Serikali na njia nyingine
ni ya hiari kwa wafanyakazi wote wakiwemo wa Serikali, Sekta binafsi na
hata wale waliojiajiri wenyewe. Kwa
wale wateja waliojiunga na mfuko huo kwa hiari wana uwezo wa kuchukua
mafao yao kwa muda mfupi tofauti na ule mfumo wa lazima wa Serikali
ambao ni lazima mteja afikie umri wa kustaafu.


Sehemu ya wajumbe katika kikao hicho.
(Na Hamza Temba – Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Rukwa @Rukwareview.blogspot.com)
0 comments:
Post a Comment