Saturday, November 23, 2013

p5 
Imeelezwa kuwa asilimia 9.1 ya Watanzania wanaugua ugonjwa wa kisukari hali ambayo huchangia na unywaji wa pombe, uvutaji wa sigara, ulaji wa vyakula usiofaa na kutokufanya mazoezi ya mwili.
Hayo yamesemwa leo  na Dk.  Omary Ubuguyu  kutoka Hospitali ya Taifa ya Muhimbili(MNH)  wakati akitoa semina kwa waandishi wea habari kuhusu ugonjwa huo leo jijini Dares Salaam.
Aliongeza kuwa asilimia ya  idadi ya watu 80 hadi 90 wanaugua ugonjwa huo duniani.
“ Unywaji wa pombe kuanzia chupa tano kwa wanaume na chupa 4 kwa wanawake huchangia kusababisha ugonjwa huu,” alisema Dk. Ubuguyu.
Kwa upande wake Mratibu wa semina  hiyo ,kutoka Mradi wa Taifa wa Kisukari, John Gardner alisema  gharama ya matibabu ya ugonjwa huo ugharimu dola za Marekani milioni  378 ya asilimia 12 ya bajeti ya afya duniani kwa mujibu wa takwimu za mwaka 2010, ambapo inaweza kufikia hadi  zaidi dola milioni 400.
 Akizungumzia kuhusu ugonjwa  huo, Dk. Zakharia Ngoma  alisema ulaji usiofaa na mtindo wa maisha huchangia kwa kiasi kikubwa . Hivyo hutumiaji  wa  vya kula vya asili , vya kuchemsha, mafuta, chumvi na sukari  kidogo , mboga za majani kwa wingi na matunda kila siku  , pamoja na vyakula vyenye virutubisho vyote husaidia kuepukana na ugonjwa huu,” alisema Dk. Ngoma.
 Aliongeza kuwa hutumiaji wa vyakula vya jamii ya kunde na visivyokobolewa husaidia kuepuka ugonjwa huu, ikiwemo kunywa maji kwa wingi na kuepuka msongo wa mawazo.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video