Monday, November 18, 2013

Mratibu wa programu ya Wafanye Watabasamu ambaye pia ni mchora vibonzo wa ITV, Nathan Mpangala (mwenye pensi nyanya), akiingia katika Kituo cha Ukuzaji Sanaa cha Koko’TEN kilicho Wilaya ya Lushoto, Mkoa wa Tanga, Jumamosi iliyopita. Mpangala, alifuatana na wachoraji wenzake Abdul King O wa gazeti la Nipashe na Said Michael wa Tanzania Daima kuendesha mafunzo ya uchoraji kwa watoto wilayani humo. Kwa matukio zaidi bofya; https://www.facebook.com/nathan.mpangala pix 2 
Mchora vibonzo na mratibu wa Wafanye Watabasamu, Nathan Mpangala akishea neno na wachoraji wa baadae katika Kituo cha Ukuzaji Sanaa cha Koko’TEN Wilaya ya Lushoto, Tanga Jumamosi iliyopita. pix 3 
Mchora katuni wa gazeti la Tanzania Daima, Said Michael almaarufu ‘Wakudata’ (kulia) nae hakubaki nyuma kushea ujuzi wake kwa watoto wa Lushoto. pix 4 
Mchora katuni wa gazeti la Nipashe, Abdul King O aka Kaboka Mchizi (kulia) akimwaga mambo kwa wachoraji katuni wa kesho katika Kituo cha Ukuzaji Sanaa cha Koko’TEN, Lushoto, Tanga, Jumamosi iliyopita. pix 5 
Ikafika wakati wa mikono kuzungumza. pix 6 
Baada ya kuwatabasamisha watoto wa Koko’TEN Art Centre, Wafanye Watabasamu ikapata nafasi ya kushangaa maajabu ya Milima ya Usambara. Pichani, mchora katuni wa gazeti la Nipashe, Abdul king O, akipata msaada wa kingo ya barabarani ili kulingana kimo na mchoraji vibonzo wa ITV, Nathan Mpangala. pix 7Mkurugenzi wa Koko’TEN Art Centre, Gadi Ramadhani (katikati) katika picha ya pamoja na Wachoraji katuni Nathan Mpangala (mwenye kaputula rangi ya Mnyama) na Abdul King O. Picha hii walipiga katika kilele cha Irente View, juu ya Milima ya Usambara. Ukifika mahala hapa, barabara ya Dar-Arusha inaonekana kama izi. pix 8 
Milima ya Usambara ina mapango yanayotaka moyo kukatiza. (Picha zote hisani ya Wafanye Watabasamu)

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video