Monday, November 18, 2013

Picture 013 
Afisa Habari wa ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali Bi. Asiatu Msuya akieleza kwa waandishi wa habari(hawapo pichani) kuhusu majukumu mbalimbali ya Divisheni ya Mikataba ikiwa ni pamoja na kutoa ushauri wa kitaalam katika masuala ya Mikataba na makubaliano yanayoihusu serikali,wakati wa mkutano uliofanyika katika ukumbi wa Idara ya Habari (MAELEZO) Leo Jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Habari (MAELEZO) Bi. Zamaradi Kawawa. Picture 028Mkurugenzi Msaidizi Divisheni ya Mikataba toka Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali Bw. Edson Mweyunge akifafanua kwa waandishi wa Habari (hawapo pichani)kuhusu utendaji kazi na mafanikio ya Divisheni hiyo katika masuala ya Mikataba,wakati wa mkutano uliofanyika katika ukumbi wa Idara ya Habari (MAELEZO) Leo Jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Habari (MAELEZO) Bi. Zamaradi Kawawa.

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI___
Ofisi ya Mwanasheria Mkuu ndiyo yenye jukumu la Kikatiba la kuishauri Serikali kwenye mambo yote ya kisheria ikiwemo masuala ya mikataba jukumu ambalo linatekelezwa kupitia Divisheni ya Mikataba.
Ili Divisheni hii, iweze kutekeleza majukumu yake, Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kwa kipindi cha mwaka 2013/2014 kwa kushirikiana na wadau mbalimbali imekuwa ikijenga uwezo wa wataalam katika kutoa ushauri wa kisheria, kuhakiki na kufanya majadiliano ya mikataba mbalimbali ya kibiashara na kimataifa yenye kuihusisha Serikali, kwa lengo la kuimarisha utendaji kazi wa Divisheni hii na kuweza kubaini matatizo kabla na hata baada ya mikataba kusainiwa ili kuweza kurekebisha  kasoro na hatimaye kuwa na mikataba yenye maslahi kwa taifa.
       i.            Ofisi imefanya mafunzo juu ya majadiliano ya Mikataba yaliyojumuisha maofisa kutoka Wizara na Taasisi za Serikali wadau mbalimbali takribani 30.
    ii.            Imeweka utaratibu wa mafunzo ya muda mrefu kwa Mawakili. Kwa mwaka huu Mawakili wa Serikali wawili wako mafunzo ni kwa ajili ya shahada ya Uzamili katika maeneo ya mafuta na gesi.
 iii.            Mwezi huu ofisi ikishirikiana na Chuo cha Uongozi imewapa mafunzo Mawakili 8 kuwajengea uwezo wa namna ya kufanya majadiliano katika maeneo mbalimbali ya Mikataba.
 iv.            Kuongeza idadi ya Mawakili katika Divisheni hii wakati wowote uwezo ukiruhusu. 
Aidha, katika kipindi cha mwaka 2012/2013 Ofisi imefanikiwa kushughulikia na kutoa ushauri wa kisheria katika mikataba 330 ambapo mikataba 295 kati ya hiyo ilihusu manunuzi ya umma na 35 ilihusu masuala ya uwekezaji, mikataba 58 ya makubaliano (MoU) na mikataba 21 ya makubaliano Baina ya nchi (Bilateral Agreements). Sambamba na hilo, Ofisi ilihudhuria katika vikao 185 vilivyohusu majadiliano ya mikataba na mahusiano ya kimataifa.
Katika kutekeleza majukumu haya, ofisi imekuwa ikikumbana na changamoto nyingi ambazo ni pamoja na:
          i.            Uhaba wa rasilimali fedha kwa ajili ya mafunzo na vitendea kazi
       ii.            Baadhi ya Taasisi na Idara za Serikali kutokuleta Mikataba au makubaliano yao kuhakikiwa kabla ya kusainiwa.
    iii.            Ufinyu wa muda kutokana na masuala ya dharura yanayohitaji ushauri wa haraka wa kisheria.
    iv.            Namba ndogo ya Mawakili wa Serikali wataalam katika maeneo mapya maalum mfano ya gesi, petroli, madini nk.
       v.            Ofisi kuhusishwa katika hatua ya kuhakiki mikataba badala ya kuhusika kuanzia kwenye hatua ya majadiliano yanayohusisha wataalam wa maeneo mengine. Mfano katika Mikataba ya manunuzi ya Umma.
    vi.            Mikataba au kazi nyingi kuletwa katika mazingira ya dharura na hivyo kutotoa mwanya wa utafiti wa kina.
KUHUSU MUUNDO MAJUKUMU YA DISISHENI YA MIKATABA.
UTANGULIZI
Divisheni ya Mikataba ni moja ya Divisheni katika Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali. Divisheni hii ya Mikataba ilianzishwa mwaka 2011, baada ya Serikali kufanya mabadiliko ya Muundo wa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali na kugawanya iliyokuwa Idara ya Madai na Sheria za Kimataifa; Idara ambayo ilikuwepo tangu kuanzishwa kwa Wizara ya Katiba na Sheria mwaka 1976.
MUUNDO DIVISHENI.
Divisheni hii inaongozwa na Mkurugenzi akisaidiwa na wakurugenzi wasaidizi wawili ambao wanaongoza sehemu mbili za divisheni; “Contracts” na  “Treaties”. Divisheni ina mawakili wa Serikali  ishirini (20)
LENGO LA DIVISHENI
Lengo kuu la Divisheni ya Mikataba ni kutoa ushauri wa Kitaalam  kuhusu masuala ya Mikataba na makubaliano yanayoihusu Serikali. Katika kutekeleza jukumu hili, divisheni kwa ujumla inafanya kazi zifuatazo;
       i.            Kuandaa na kushauri juu ya mikataba na Makubaliano mengine  yanayoihusisha Serikali,
    ii.            Kutoa ushauri wa Kisheria kwa Serikali  kuhusiana na makubaliano ya Kikanda,
 iii.            Kutoa ushauri wa kisheria kwa Serikalki kwenye majadilano ya mikataba yanayoihusisha Serikali au katika mikataba na makubaliano na majadilano mengine ambayo Serikali ina manufaa,
 iv.            Kutoa ushauri wa kisheria kwa Idara na taasisi za Serikali kwenye mikataba na makubaliano mengine ambayo Serkali ina manufaa.
Aidha kama tulivyosema awali, Divisheni hii imegawanyika katika sehemu mbili. Kila moja ya sehemu hizi ina kazi maalum inazozitekeleza. Sehemu  ya mikataba ya kibiashara (Contracts) inafanya kazi zifuatazo:
       i.            Kutoa ushauri wa kisheria kweye majadiliano ya mikataba na makubaliano mengine ya kibiashara ambayo yanayoihusisha serikali mfano Madini, miundombinu nk.
    ii.            Kutoa ushauri wa kisheria kwenye mikataba na nyaraka nyingine za kisheria ambazo zinaihusisha au Serikali ina manufaa.
 iii.            Kufanya utafiti wa kisheria kuhusu masuala yanayohusu mikataba ya Serikali.
 iv.            Kutoa ushauri wa Kisheria kwa idara na taasisi za Serikali kuhusu utekelezaji wa Mikataba yenye manufaa kwa Serikali.
    v.            Kuhakiki na kushauri juu ya mikataba ya manunuzi.
 vi.            Kuandaa maoni ya kisheria pale ambapo kuna masharti ya awali katika utekelezaji wa mikataba ya mikopo kutoka taasisi mabali mbali za kifedha.
vii.            Kushauri shirika la ubinafsishaji (CHC) kwenye mambo ya ubinafsishaji wa makampuni yaliyochini yake na utekelezaji wa mikataba yake.
viii.            Kushauri juu ya mikataba yote ya Serikali kabla ya kusainiwa. 
Divisheni hii sehemu ya  “ Treaties” inafanya kazi zifuatazo”
       i.            Kupitia na kutoa ushauri wa kisheria juu ya mikataba ya kikanda, bilateral na multilateral.
    ii.            Kutoa ushauri wa kisheria kwa Serikali kwenye mikataba na majadilano ya Mikataba ya Kimataifa ,
 iii.            Kutoa ushauri wa kisheria kuhusu mahusianao na kazi za taasisi za jumuiya ya kimataifa mfano; Umoja wa Mataifa, EAC, SADC, katika masuala ambayo yanahitaji kutoa msimamo wa Serikali.
 iv.            Kufanya utafiti wa kisheria kuhusu mikataba ya Kimataifa.
    v.            Kutoa ushauri wa kisheria kwa Wizara, Taasisi za Serikali na kwa umma kuhusu masuala ya makubaliano ya kimataifa.
 vi.            Kushauri Wizara na taasisi za Serikali kuhusu mikataba ya kimataifa inayohitaji ridhaa ya bunge kabla ya kusainiwa,
vii.            Kushauri Wizara na Taasisi zinazojitegemea kuhusu utekelezaji wa Mikataba ya Kimataifa.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video