Saturday, November 23, 2013

RC NA WATOTODARASANI 
Hao ni baadhi ya Wanafunzi ambao hawapo katika mfumo rasimu wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa KATAVI  Dkt Rajabu Lutengwe aliyefika kuwatembelea wakiwa darasani huko kijiji cha Luchima kitongoji cha kata ya maji moto.
Watoto hao wa wafugaji wa kabila la kisukuma,  wazazi wao wameondolewa kutoka maeneo yaliyokatazwa kuishi na sasa wamehamia maeneo ya kijijini, lakini  eneo hilo halina  shule ya Msingi ingawa umri wao unaruhusu elimu  ya Msingi na wengi wao wana miaka kumi na mbili.
Kwa sasa wanapata elimu kupitia mfumo usio rasmi , hawajaandikishwa, vyumba vya  madarasa hakuna,madawati shida  na huduma nyinginezo hapo wanasomea nje iwapo mvua ikinyesha hatima yao haijulikani juhudi za makusudi zinahitajika kuokoa kizazi hicho. Shule hiyo isiyo rasmi iko umbali wa kilometa takribani 40 kutoka makao makuu ya kata.
Picha na Kibada Wakibada, -Mlele- Katavi

Na Kibada Kibada  -Mlele Katavi
Mkuu wa Mkoa wa Katavi Dkt Rajabu Rutengwe amemaliza ziara yake Katika Halmashauri ya Wilaya ya Mlele na kutoa  maagizo kwa watendaji  wa Vijiji na Kata kuwataka wasimamie utekelezaji wa shughuli za maendeleo   ili kuwalete wananchi maendeleo ya haraka .
Amesema kushindwa kusimamia maagizo ya viongozi yanayotolewa katika mkoa ni utovu wa nidhamu,  haina maana kuendelea kupokea mshahara wa serilaki wakati huwatimizi wajibu waliokabidhiwa na serikali kuhakikisha wanawaletea wananchi wa Mkoa wa Katavi Maendeleo.
Alisema kuwa Moja ya mikakati ya mkoa na malengo iliyojiwekea na kuhimiza watendaji wote wa Vijiji , Kata , Tarafa , Halmashauri na Wilaya ni kuhakikisha wanatekeleza ufyatuaji wa Tofali milioni moja kwa kila kijiji, watoto kupata chakula shuleni, kuondoa tatizo la madawati, kufuta utoro mashuleni, kuongeza kiwango cha ufaulu kufika lengo la mkoa la asimilia sitini na lengo la Taifa pia asilimia Sitini, kutosikia kuwa watoto wameacha shule kutokana na mimba , utoro mashuleni, ujenzi wa maabara,hosteli vyumba vya madarasa na Nyumba za walimu pamoja na kulima kilimo chenye  tija kinachomkomboa mwananchi, lakini hayo yote hayatekelezwi .
Ziara hiyo imemchukua Dkt Rutengwe takribani wiki mbili kwa kuanza kutembelea Halmashauri ya wilaya ya  Mpanda  na kukagua miradi  mbalimbali ya maendeleo katika Kata za Karema, Ikola, Kapalamsenga, Mwese., Zote zipo Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda .
Kata nyingine alizotembelea ni  Kata  ya Sibwesa,Katuma,  Kabungu, Mpanda, Mpandandogo na Mishamo ambapo alifanikikiwa kukagua ujenzi wa miradi ya kilimo ujenzi wa  ghala katika kijiji cha Mwese, Msitu wa asili uliohifadhiwa katika kijiji cha Mwese unaotumiwa na wananchi wa Mwese kwa matumizi ya kuhifadhi mazingira.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video