Tuesday, November 19, 2013

Na Mahmoud Zubeiry, Dar es Salaam
MGOGORO mwingine unakuja Simba SC, katika wakati ambao klabu inahitaji kujipanga ili kurejesha makali yake yaliyopotea kwa mwaka wa pili sasa.
Baadhi ya Wajumbe wa Kamati ya Utendaji ya Simba SC, walikutana jana usiku katika kikao bila ya Mwenyekiti wao, Alhaj Ismail Aden Rage na kuchukua maamuzi mazito.
Maamuzi hayo ni; kwanza kumsimamisha Mwenyekiti wao, Rage kwa madai hawana imani naye na pili kuwasimamisha makocha wa timu hiyo, Alhaj Abdallah Athumani Seif ‘King Kibadeni’ na Msaidizi wake, Jamhuri Mussa Kihwelo ‘Julio’, kwa madai hawaridhishwi na uwezo wao.
Mzee umechafua hali ya hewa; Joseph Itang'are Kinesi kushoto akiwa na Geoffrey Nyange 'Kaburu' kulia jana Uwanja wa Karume, saa chache kabla ya kwenda kufanya kikao cha kumng'oa Rage

Baada ya hayo, Kamati pungufu ya Utendaji, bila ya Mwenyekiti aliyechaguliwa na wanachama kuongoza klabu, ikaamua kumfanya Suleiman Abdallah Matola ‘Veron’ kuwa kocha Msaidizi wa kocha mpya, atakayetangazwa Desemba 1.
Matola ambaye kwa sasa ni kocha wa Simba B, ataanza kuiandaa timu kwa ajili ya mzunguko wa pili wa Ligi Kuu na Kombe la Mapinduzi wakati kocha mpya wa kigeni akisubiriwa.
Aidha, Joseph Itang’are ‘Kinesi’ ambaye alichaguliwa kama Mjumbe wa Kamati ya Utendaji, akajibebesha jukumu la kukaimu nafasi ya Rage, wakati tayari anakaimu nafasi ya Makamu Mwenyekiti, iliyoachwa wazi na Geoffrey Nyange ‘Kaburu’ aliyejiuzulu mapema mwaka huu.
Kikao kilifanyika jana Jumatatu, wakati Jumapili Rage alifanya zoezi la kusajili wachezaji wawili wapya, kiungo Awadh Juma na mshambuliaji Ally Badru, wote kutoka Zanzibar.
Kinesi alipoulizwa na Waandishi wa Habari kuhusu Rage kutokuwepo kwenye kikao cha jana, akajibu amesafiri, lakini swali linakuja kwa nini kikao kisifanyike akiwepo na kama kuna tuhuma akazijibu?
Lakini pia, Kinesi hakuweza kuwaambia Waandishi wa Habari sababu ya kumsimamisha Rage, zaidi ya kusema tu hawana imani naye.
Mamia ya wanachama walionyesha imani kwa Rage na wakamchgua kwa kura nyingi kuwa Mwenyekiti wao, iweje leo watu wanne au watano wachukue maamuzi mazito dhidi yake?
Wazi hapa Kinesi na wenzake waliokutana kwenye kikao cha jana waneleta mgogoro ambao utazidi kuiyumbisha Simba SC na kuifanya pia izidi kuboronga katika Ligi Kuu.       
Simba SC ina tatizo la uongozi na hilo limeonekana wazi katika kipindi chote cha utawala wa Rage kuwapo madarakani, lakini kitendo cha baadhi ya Wajumbe kufikia maamuzi mazito jana ni ukaribisho wa tatizo lingine kubwa ndani ya klabu.
Rejea mapema mwaka huu wakati baadhi ya wanachama walipofanya Mkutano na kutangaza kuung’oa uongozi mzima wa Rage, baadaye likatokea kundi kubwa la wanachama kumpokea Uwanja wa Ndege kwa maandamano ya kishujaa akitokea India na kutibiwa na kusistiza huyo ndiye Mwenyekiti wao.
Na hali kama hii ndiyo inatarajiwa kujirudia sasa ila katika makali zaidi, kwa sababu safari hii si wanachama waliofanya maamuzi, bali viongozi wenzake Rage. Yetu macho na masikio huko Msimbazi. 

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video