Sunday, November 24, 2013


Dar es Salaam. Muuguzi aliyejitoa damu kuokoa maisha ya mjamzito Sista Hyasinta Baruti na mume aliyemsindikiza mkewe kila alipohudhuria kliniki wakati wa ujauzito Elia Mwumbui ni miongoni mwa Watanzania waliopewa tuzo ya kuboresha afya ya mama na mtoto.
Tuzo hiyo iliyoandaliwa na Taasisi ya Madaktari Wahitimu Vyuo Vikuu vya Tanzania (THPI), pia ilitolewa kwa Dk Faraja Mpwapwacha wa Lindi kwa rekodi ya mama au mtoto kutokufa kwa miaka miwili wakati akizalisha.
Wengine waliopata tuzo hiyo ni marais wastaafu, Ali Hassan Mwinyi na Benjamini Mkapa pamoja na Rais Jakaya Kikwete na mkewe Mama Salma Kikwete.
Pia tuzo hiyo ilienda kwa Mwenyekiti wa IPP, Dk Reginald Mengi kutokana na mchango wake katika mapambano ya saratani ya matiti.
Akizungumza katika hafla ya utoaji tuzo hizo, Makamu wa Rais, Dk Mohammed Gharib Bilal ambaye alikuwa mgeni rasmi alisema, nchi isipokuwa na raia walio radhi kusimamia uhai wa wenzao nchi hiyo ni sawa na jangwa hasa katika suala la afya.
 Pia   Dk  Bilal  amesema, ushirikiano wa wadau mbalimbali wa sekta ya afya utapunguza vifo vya mama na mtoto sambamba na maboresho ya utoaji wa huduma hiyo nchini.
“Kama kila mmoja wetu asipokuwa makini kusimamia uhai wa wenzake nchi hiyo ni sawa na jangwa, hivyo tunawaomba wanaohusika na sekta ya afya watekeleze wajibu wao ipasavyo” alisema Dk Bilal
Naye Mkurugenzi wa THPI, Dk Telesphory Kyaruzi alisema vifo vya mama na mtoto vimepungua ukilinganisha na miaka ya nyuma.
Alisema jitihada hizo zitaendelea kufanikiwa ikiwa madaktari wazawa watakuwa wazalendo na kufanya kazi nchini ili kuokoa maisha ya Watanzania wanaopoteza uhai kwa kukosa huduma.
 CHANZO: MWANANCHI

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video