Tuesday, November 19, 2013


Na Gladness Mushi, Arusha
CHUO cha uasibu Arusha(IAA)kimesema kuwa kimefanikiwa kukusanya kiasi cha zaidi ya Bilioni Moja  kwa mwaka tofauti na hapo awali ambapo walikuwa wanakusanya kiasi cha Milioni 20 kwa mwaka jambo ambalo limesababishwa na ongezeko kubwa la wanafunzi .
Hayo yamebainishwa na mkuu wa chuo hicho  ambaye ni Profesa Johanes Monyo wakati akiongea kwenye maafali ya nne ya chuo hicho yaliyofanyika chuoni hapo mapema jana.
Profesa Monyo,alisema kuwa ongezeko la fedha hizo ni kutokana na kuwepo kwa wanafunzi wengi tofauti na miaka ya nyuma ambapo  na hivyo ongezeko hilo limesababisha mapato nayo kuweza kukua kwa haraka sana.
Alifafanua kuwa kinachosababisha waweze kupata ongezeko kubwa la wanafunzi tena kwa kila mwaka ni kwa kuwa chuo hicho kinakugusa nyanja mbalimbali za elimu wanayoitoa lakini pia wanashirikiana na vyuo vilivyoendelea duniani katika kuwasaidia wanafunzi.
Alisema ushirikiano baina yao na vyuo ambavyo vimeemdelea duniani kumesababisha ongezeko lakini hata uwezo wa kufanya kazi kwa baadhi ya wahitimu wa chuo hicho na hivyo kusababisha hata nchi ya Tanzania kuweza kupata sifa lukuki mahala pa kazi.
Kutokana na ongezeko hilo la wanafunzi katika Chuo hicho cha uasibu Arusha alidai kuwa bado kinakabiliwa na changamoto lukuki ambazo kama zingeweza kutatuliwa kwa haraka basi watanzia walio wengi zaidi wangeweza kunufaika na chuo hicho na hivyo kusababisha hata matokeo ya  haraka.
Alitaja changamoto hizo kuwa ni pamoja na uhaba wa majengo ya kutosha ambapo majengo yaliopo kwa sasa bado hayawezi kuwatosheleza wanafunzi wote ukilinganisha na ongezeko kubwa la wanafunzi wanaohitaji kujiunga na chuo hicho kwa ajili ya kuweza kupata elimu. 
Pia alimalizia kwa kutaja changamoto nyingine kuwa ni pamoja na ukosefu wa wahadhiri wa kutosha kwani waliopo kwa sasa bado hawatoshelezi mahitaji ya chuo hicho.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video