Friday, November 22, 2013

gurumo muhidin-1 
GWIJI wa muziki wa dansi, Muhidin Maalim Gurumo ameugua ghafla mapema leo na kulazwa Hospitali yaTaifaMuhimbili.
Wajumbe wa Kamati ya maandalizi yaTamasha la Gurumo, Juma Mbizona Said Mdoe, waliokuwepoMuhimbili, wameuambia mtandao huu kuwa mwimbaji huyo mkongwe alipatwa na tatizo la shinikizo la damu na hali ikawa mbaya kabla ya kukimbizwa hospitalini hapo. 
Wamesema kwasasa hali yake inaendelea vizuri na amelazwa katika wodi ya Mwaise la namba 1. 
Wajumbe hao wamesema siku chache zilizopita, Gurumo alikuwa kwenye afya njema na hata siku ya Jumanne alihudhuria kikao cha kamati hiyo kilichofanyika Vijana Social Hall Kinondoni. 
Aidha, wajumbe hao wamedai kuwa kwamujibu wa mke wa Gurumo, Bi Pili, ni kwamba hata jana mwimbaji huyo alikuwa hana tatizololote na alifanya mizunguko yake bila ya mikwaruzo yoyote.
Mwenyekiti wa kamati ya maandalizi ya tamasha la Gurumo, Bi Asha Baraka amewataka wapenzi wa muziki kuwa watulivu kwa vile hali ya mwanamuziki huyo aliyeitumikia fani kwamiaka 53, inaendeleavizuri. 
Tamasha la Gurumo limepangwa kufanyikat arehe 14 mwezi ujao katikav iwanja vya TCC Club Chang’ombe.
Tumuombee dua mzee wetu Gurumo.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video