Na Gladness Mushi, Arusha
Katika hali isiyokuwa ya kawaida mkuu wa mkoa wa Arusha Magesa Mulongo ametangaza utaratibu mpya kwa wakurugenzi ambapo kuanzia sasa wataomba ruhusa za kwenda nje ya wilaya au mkoa kwa sababu maalumu
Katika hali isiyokuwa ya kawaida mkuu wa mkoa wa Arusha Magesa Mulongo ametangaza utaratibu mpya kwa wakurugenzi ambapo kuanzia sasa wataomba ruhusa za kwenda nje ya wilaya au mkoa kwa sababu maalumu
Aidha
utaratibu huo unakuja mara baada ya mkuu huyo kudai kuwa wakurugenzi
wote wa jiji la arusha wanaweza kuongeza ufanisi wa maendeleo lakini pia
wakapunguza kasi ya maendeleo
Mulongo
aliyasema hayo mapema wiki hii wakati akiongea na viongozi wa vijiji
kutoka maeneo mbalimbali jijini hapa huku lengo halisi la kukutana nao
likiwa ni kujadili namna ya kuongeza mafanikio ya miradi iliopo kwenye
ngazi za vijiji
Mulongo alisema kuwa kwa wakurugenzi wote wa Jiji la Arusha kuanzia
sasa wataomba ruhusa maalumu kwa wakuu wa wilaya lakini pia kwenye ofisi
yake ili kupunguza tatizo la kutoka nje ya ofisi kila mara
Aidha
alidai kuwa utaratibu huo wa kuomba ruhusa utaweza kupunguza kasi ya
safari ambazo hazina tija kwenye Halmashauri hivyo basin itaweza
kuruhusu maendeleo kwa wananchi kwa haraka sana tofauti na sasa ambapo
wakitaka kwenda mahala popote pale wanakwenda.
Wakati
huo huo pia alisema kuwa mbali na kuomba ruhusa kwa wakuu wa wilaya
lakini pia hata katika ofisi yake ni lazima pia watambue wana nafasi
kubwa sana ya kuwasaidia wananchi na wala sio kukaa maofisini kama
wanavyofanya baadhi yao kwa sasa
Alisema kuwa wakurugenzi kwa kushirikiana na wakuu wa idara sasa wanapaswa kutembea kwa wananchi zaidi kuliko kuipenda ofisi na endapo kama watakiuka agizo hilo ambalo linaenda katika wilaya zote za Jiji la Arusha basi watachukuliwa sheria kali
Alisema kuwa wakurugenzi kwa kushirikiana na wakuu wa idara sasa wanapaswa kutembea kwa wananchi zaidi kuliko kuipenda ofisi na endapo kama watakiuka agizo hilo ambalo linaenda katika wilaya zote za Jiji la Arusha basi watachukuliwa sheria kali
Pia
aliwataka viongozi kuanzia ngazi ya Kitongoji kuhakikisha kuwa wanaweka
utaratibu wa kutambua miradi iliopo kwenye kata ili kuweza kuwabana
baadhi ya viongozi wa Serikali ambao wanatumia miradi hiyo kwa ajili ya
kujinufaisha.
0 comments:
Post a Comment