Na Baraka Mpenja, Dar es salaam
HATIMAYE
Ashanti United `Watoto wa jiji` waanza kuonja ladha ya ushindi katika
mikikimikiki ya ligi kuu soka Tanzania bara baada ya jioni ya leo
kuibuka na pointi tatu nyingine muhimu mbele ya Tanzania Prisons
`Wajelajela` kutokana na ushindi wa mabao 2-1 uwanja wa Azam Complex,
Chamaz, nje kidogo ya jiji la Dar es salaam.
Bao
la ushindi limetiwa kimiani dakika za lala salama, lala kwa buriani
ambazo hazimruhusu hata kuku kumeza punje ya mchele na Mwinyi Ally.
Ally
aliyetokea benchi dakika ya 83 kuchukua nafasi ya Fakhi Hakika,
alipachika bao hilo lililoleta raha kubwa kwa mashabiki wa Ashanti ambao
walishaanza kuvunjika moyo baada ya kutokea pukurushani katika lango la
maafande hao wa Magereza wenye makazi yao jiji Mbeya.
Hadi
mapumziko, timu hizo zilikuwa zimechoshana nguvu kwa kuburuzana bao 1-1
ambapo Prisons walitangulia kupata bao dakika ya nne kupitia kwa John
Matei na beki Tumba Sued akaisawazishia Ashanti dakika ya 21.
Kiujumla
Prisons inayofundishwa na kocha mkuu Jumanne akisaidiwa na mchezaji wa
zamani wa klabu hiyo, Osward Morris walianza mchezo huo kwa kutandaza
kabumbu safi hasa dakika 15 za mwanzo, lakini baadaye mambo yakawageukia
kabisa na kama Ashanti wangekuwa makini kubadili nafasi muhimu za
kufunga kuwa magoli, basi wangemaliza dakika 45 wakiwa kifua mbele.
Kipindi
cha pili, Ashanti chini ya kocha wake, Nico Kiondo iliongeza kasi ya
mashambulizi langoni mwa Prisons, lakini kukosekana kwa umakini wa
washambuliaji wake kuliwagharimu na kushindwa kuweka gozi kambani.
Kwa ushindi huo, Ashanti inatimiza point nane baada ya kucheza mechi tisa na sasa inasogea hadi nafasi ya 10 kutoka ya 13.
Kikosi cha Ashanti United leo: Daudi Mwasongwe, Hussein Mkongo/Anthony Matangalu dk46, Jaffar Gonga, Tumba Sued, Samir Ruhava, Iddi Silas, Mussa Nampaka, Fakhi Hakika/Mwinyi Allydk83, Paul Maona, Joseph Mahundi na Lusajo Mwakyusa/Hussein Swedi dk51.
Kwa ushindi huo, Ashanti inatimiza point nane baada ya kucheza mechi tisa na sasa inasogea hadi nafasi ya 10 kutoka ya 13.
Kikosi cha Ashanti United leo: Daudi Mwasongwe, Hussein Mkongo/Anthony Matangalu dk46, Jaffar Gonga, Tumba Sued, Samir Ruhava, Iddi Silas, Mussa Nampaka, Fakhi Hakika/Mwinyi Allydk83, Paul Maona, Joseph Mahundi na Lusajo Mwakyusa/Hussein Swedi dk51.
Prisons:
Beno David, Salum Mashaka, Laurian Mpalile, Lugano Mwangama, Nurdin
Issa/Frank William dk82, Omega Seme, John Matei, Freddy Chudu, Peter
Michael, Hassan Isaka/Jumanne Elfadhil dk71 na Julius Kwanga/Jeremiah
Juma dk47.
0 comments:
Post a Comment