Thursday, October 31, 2013

JESHI la polisi jijini Mbeya limesema kamwe halikubaliani na vurugu zinazojitokeza kwa mashabiki wa kandanda mkoani humo katika michezo mbalimbali ya ligi kuu soka Tanzania bara na ligi nyingine.
Kamishina msaidizi wa Polisi ambaye pia ni mkurugenzi wa kitengo cha upelelezi mkoani Mbeya na Kaimu kamanda wa polisi, Robert Mayala ameuambia mtandao wa MATUKIO DUNIANI kuwa juzi mashabiki wanaosadikika kuwa wa Mbeya City walishambulia gari za Tanzania Prisons eneo la Hoteli ya Rift Valley wakati wanarudi kambini na kupasua vioo sanajari na kuwajeruhi baadhi ya wachezaji akiwemo Lugano Mwangamba.
“Michezo ni furaha na sio vurugu, mashabiki wa Mbeya City hawakuwa na sababu ya kufanya vurugu kwani walikuwa wameshinda mchezo huo, na mpaka kufikia jana watu sita tunawashikilia na leo hii (jana) tunawapeleka mahakamani kusomewa mashitaka. Kwa pamoja tunalaani vurugu hizi na tunaahidi kuchukua hatua kali”. Alisema Kamishina msaidizi wa Polisi Robert Mayala.
IMG-20131029-WA0080 
Kamishina msaidizi Mayala aliongeza kuwa Kushambulia wachezaji au mashabiki ni kosa kama makosa mengine kisheria, na wao watahakikisha wanaohusika wanafikishwa mbele ya vyombo vya dola.
“Kama tutaliachia hili kuendelea kutokea, watu wengi wataacha kwenda viwanjani kushuhudiwa mpira, na tutapotosha zana halisi ya mpira ambao siku zote ni burudani na amani”. Alisema Kamishina Mayala.
Wakati jeshi la polisi likisema hilo, tayari uongozi wa Tanzania Prisons, `Wajelajela` kupitia kwa katibu wake mkuu, Inspeckta Sadick Jumbe wameeleza kusikitishwa na vitendo walivyofanyia na baadhi ya mashabiki wa Mbeya City.
Jumbe alisema wao wameshakubali matokeo bila tatizo lolote, lakini hawakubaliani na vurugu walizofanyiwa, hivyo wamesema wanaandika ushahidi wa kimaandishi ambao watawasilisha shirikisho la soka nchini Tanzania TFF.
“Kama Mbeya City wamefikia hatua ya kutufanyia vurugu ndugu zao, je, itakuwaje kwa wageni?, Waliwafanyia vurugu wakongwe Yanga, jana (juzi) sisi, na Ashanti wanakuja Mbeya, hawatawafanyia vibaya zaidi?. Alihoji Jumbe.
IMG-20131029-WA0082
Vioo nyang`anyang`a: Gari la Wajelajela Tanzania Prisons lilipigwa mawe na baadhi ya wachezaji kujeruhiwa
Inspeckta huyo alisema ana uwezo kisheria wa kuwaruhusu vijana wakapambana na watu hao, lakini kama akifanya hivyo atafanya mambo yawe mabaya kwa wapinzani wao kwani nguvu wanazo na uwezo wa mapambano kijeshi wanao.
“Nitoe rai kwa Mheshimiwa Rais wa TFF, Jamal Emily Malinzi kuanza uongozi wake kwa kuwachukulia hatua kali Mbeya City, wao tu ndio wanapenda vurugu. Ipo siku hatutawavumilia”. Alisema Inspecta Jumbe.
Nao Mbeya City kupitia kwa katibu wake mkuu, Emmanuel Kinde wamekanusha kuhusika na tukio hilo, bali amesema kuwa ni mpango uliopangwa na Prisons ili kufanya vurugu.
Kinde alisema awali walikaa na jeshi la polisi na kukubaliana kuwa mwisho wa mechi timu zote zisindikizwe na polisi, lakini haikuwa hivyo.
Pia walisikia kuwa kuna watu wana mpango wa kufanya vurugu na waliwaambia polisi, lakini hawakulichukulia uzito.
“Sisi tunajua Prisons wanaeneza propaganda zao ili wahame Mbeya, ni mpango wa muda mrefu wa kutaka kuuhama uwanja wa Sokoine, wao waondoke na sisi tutabaki. Na ninavyokuambia hivi , kuna watu wamekamatwa sehemu tofauti kabisa na uwanjani kwa kwa madai ya kuhusika na vurugu na wanapelekwa mahakamani kesho (leo)’. Alisema Kinde.
Kinde aliongeza kuwa ni wakati wa matatizo ya mpira kutatuliwa kwa misingi ya kimpira, hivyo amewataka mashabiki wao kuwa watulivu wakati huu, pia ametoa wito kwa watu wa usalama kuwa makini na upotoshwaji wa Taarifa.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video