Wednesday, October 16, 2013

Moja ya soko maarufu hapa mjini mpanda ambalo ni tegemeo kwa wakazi wa mjini mpanda hususani wakazi wa majengo. soko hilo liko  majengo mapya kata ya KawanjeseH/Mji wa Mpanda,  pia   so limezungukwa na uchafu kila kona huku pembeni kukiwa na Dampo la kumwanga uchafu eneo ambalo siyo rasmi na mamlaka husika kila siku zinapita na kuuangalia, na mbaya zaidi soko hilo liko mbele ya ofisi ya mtendaji wa  kata, mtaa wa kawajense na ofisi ya afisa afya ngazi ya kata anaangalia bila kuchukua hatua zozote za kutoe elimu kwa jamii na pengine sheria ichukue mkono wake. 
Dampo la kutupia uchafu likiwa mbele ya soko la kuuzia mboga mboga na vyakula aina ya matunda katika mji wa mpanda eneo la kawajense hali ambayo ni hatari kwa watumiaji wa vyakula kutoka katika soko hilo. Na iwapo hatua za makusudi hazitachuliwa kuthibiti hali hiyo hasa wakati tunapoelekea kuanza kunyesha kwa msimu wa mvua ni hatari kwa wananchi kwani wanaweza kukumbwa na magonjwa ya mlipuko kama kuhara, kipindupindu na  matokeao yake kupoteza maisha.
  Hali ya kuzingatia usafi ni jukumu la mamlaka husika kuliangalia  kwa mapana na marefu na kuchukua hatua za makusudi kuelimisha jamii kabla ya kutokea madhara zaidi. Heri kuzuia kuliko kutibu,  kazi kwenu wenye dhamana. MAMA NA MWANAE WAKICHOMA MKAA 
Mama na Mwana wakijitafutia riziki kwa kuchoma mkaa na kujikuta wakijihusisha na ukataji wa miti kiholela, kiukweli, kama tabia hii itazidi kushika kasi zaidi na zaidi, Mpanda wanakaribisha ukame huku wakijiona kabisa. Suala la utunzaji wa mazingira ni kuanzia kwa wananchi ambao wanapaswa kuelemishwa na kukumbushwa, hadi mamlaka zinazohusika, `Tunza mazingira yakutunze`.MITI KUKATWA HOVYO 
Uharibifu wa mazingira unachangiwa na mambo mengi na pengine umasikini na kutokuwa na uelewa wa kutosha kutokana na athari za uharibifu huo hasa umasikini kama mama huyo ambaye jina lake halikuweza kufahamika akiwa na mwanaye wakichoma tanuru la mkaa ili kujitafutia riziki,  mkono uweze kwenda kinywani kwa kuwa hana jnsi nyingine ya kupata kipato badala yake anategemea kuchoma mkaa kama alivyokutwa na kamera katika kijiji cha Sungamila Kat ya Kasokolo H/Wilaya ya Nsimbo Wilaya ya Mlele.
PICHA NA KIBADA WAKIBADA-MPANDA-KATAVI

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video