Tuesday, October 22, 2013

Na Baraka Mpenja , Dar es salaam
UONGOZI wa klabu ya Wekundu wa Msimbazi, Simba SC wamewataka wanachama na mashabiki wao kuendelea kujenga imani kubwa kwa kocha wao mkuu ambaye ni mzawa, Alhaji Abdallah Athumani Seif ` King kibadeni Mputa` kwani anao uwezo wa kuwafikisha mbali zaidi.
Mwenyekiti wa klabu hiyo, Alhaji Ismail Aden Rage amesema kuwa mradi wa kuijenga upya Simba unahitaji muda na imani kwa kocha Kibadeni kwani ndiye kocha bora pekee hapa nchini kwa muda wote.
“Kiukweli hakuna kocha yeyote, awe wa kigeni au nyumbani aliyewahi kuifikisha timu yoyote fainali za kombe la washindi barani Afrika mnamo mwaka 1993 zaidi ya Kibadeni. Pia hakuna mchezaji yeyote aliyefunga mabao matatu (Hat -Trick) mpaka leo katika mchezo wa watani wa jadi, zaidi ya Kibadeni mnamo mwaka 1977 ambapo tuliwafunga Yanga 6-0. Kwahiyo Kibaden ndiye kocha bora na anahitaji muda zaidi kwani anaweza sana”. Alisema Rage.
rage 1
Bosi: Mwenyekiti wa Simba Sc, Alhaji Ismail Aden Rage atakuwepo Mkwakwani Tanga kesho kuwaongoza vijana wake

Rage ambaye ni mbunge wa Tabora mjini (CCM) alisema uongozi wa klabu hiyo una imani kubwa na kocha wao, na kiwango ambacho Simba walikionesha kataika mchezo wa jumapili dhidi ya Yanga na kuambulia sare ya 3-3 wakisawazisha mabao hayo kipindi cha pili inadhihirisha ubora wa Kibadeni, hivyo wanachama lazima wamwamini zaidi.
Rage ambaye kabla ya mchezo wa Yanga alitamba klabu yake ya Simba ingeifunga Yanga 6-0, lakini mpaka dakika 45 za kipindi cha kwanza zinamalizika, mnyama alikuwa nyuma kwa mabao 3-0, lakini walikuja juu na kusawazisha yote kipindi cha pili.
Kinesi
Mkali wa rekodi Tanzania: Mfungaji wa mabao matatu pekee kwenye michezo ya watani wa jadi (Hat- Trick) , Abdallah Kibadeni

Pia Rage alisema kuongoza Simba SC ni kazi kubwa kwani kuna watu wana malengo ya kuendeleza timu na wengine ndani yake wana nia ya kuleta mambo ya kuharibu timu, hivyo akasisitiza kuwa lazima wanachama, viongozi na wachezaji waungane kwa pamoja.
Wakati Rage akisema hayo, nayo Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) inaendelea kesho (Oktoba 23 mwaka huu) kwa mechi tatu; ambapo Yanga itaikaribisha Rhino Rangers katika mchezo utakaofanyika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Coastal Union inaikaribisha Simba katika mechi itakayopigwa Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga na kuchezeshwa na mwamuzi Dominic Nyamisana kutoka Dodoma.
Tanzania Prisons ambayo imepoteza mechi mbili zilizopita ugenini dhidi ya Ashanti United na Simba inarejea uwanja wake wa Kumbukumbu ya Sokoine kwa kuikaribisha Kagera Sugar.
Nayo Ligi Daraja la Kwanza (FDL) inaendelea kesho (Oktoba 23 mwaka huu) kwa mechi moja ya kundi A itakayozikutanisha Tessema na Villa Squad kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume jijini Dar es Salaam.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video