Saturday, October 19, 2013


Na Baraka Mpenja, Dar es salaam
AZAM FC imemtupa pembeni Mnyama Simba kukalia usukani wa ligi kuu soka Tanzania bara baada ya jioni ya leo kuibuka na ushindi wa 1-0 dhidi ya JKT Oljoro dimba la Sh. Amri Kaluta Abeid jijini Arusha, huku shukurani kubwa zikienda kwa Khamis Mcha `Vialli` aliyefunga bao hilo pekee dakika ya 67.
Azam fc wamefikisha pointi 20 wakiizidi Simba SC pointi 2 baada ya kushuka dimbani mara 10, lakini wanawazidi wanamsimbazi mechi moja kwani wao wamecheza mechi 9.
Afisa habari wa klabu hiyo, Jafar Idd Maganga ameuambia mtandao wa MATUKIO DUNIANI! kuwa mchezo huo ulikuwa mgumu sana ingawa waliingia kwa lengo la kupata ushindi wa kihistoria kwa maana ya kubarizi kileleni kwa muda wakisubiri matokeo ya mechi ya kesho.
“Tumekwea kileleni kwa kufikisha pointi 20, tunarudi Dar es salaam kesho na kuingia kambini moja kwa moja. Lengo letu ni kuendelea kukalia nafasi ya juu. Pia kwa niaba ya uongozi wa Azam, nawashukuru sana wachezaji wetu kwa kuwa wapiganaji wa kweli”. Alisema Jafar. 1239581_432061306914560_864943343_n 
Huko Mbeya katika uwanja wa Sokoine, wenyeji wa uwanja huo, klabu kali ya Mbeya City imeibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya maafande wa jeshi la kujenga taifa kutoka mkoani Pwani, JKT Ruvu.
Bao la ushindi wa Mbeya City limefungwa na mshambuliaji hatari, Jeremiah John dakika ya 36 na kuisaidia timu hiyo kupanda nafasi ya pili nyuma ya Azam fc ikifikisha pointi 20 lakini wamezidiwa wastani wa magoli ya kufunga na kufungwa.
IMG_7861 
Coastal Union licha ya kusajili majembe ya nguvu mambo bado magumu sana
Mechi nyingine ilikuwa huko Manungu Complex mkoani Morogoro baina ya wenyeji wa dimba hilo,  Mtibwa sugar dhidi ya Mgambo JKT, na dakika tisini za mchezo huo zimemalizika kwa wanajeshi hao kula kipigo cha mbwa mwizi cha mabao 4-1 na kuendelea kushikilia rekodi ya kufungwa mabao mengi mpaka sasa msimu huu.
Mabao yametiwa kimiani na Shaaban Nditi dakika ya 17, Juma Luizio dakika ya 25 na 60 na Salum Mkopi dakika ya 61, wakati la Mgambo lilifungwa na Malimi Busungu dakika ya 83.
Baada ya mchezo huo, Meneja wa klabu ya Mtibwa, David Bugoya ameongea na mtandao huu na kusema siku ya leo kikosi chao kimepiga soka safi zaidi.
“Ukiiangalia Mtibwa kwa sasa, kiukweli inapendeza sana, soka lake ni la uhakika. Tutaendelea kujipanga zaidi ingawa ligi yenyewe ngumu sana”. Alisema Bugoyo.
Nao Ashanti United `watoto wa jiji` ambao kwa siku za karibuni wameamka kutoka usingizini, wamelazimisha sare ya 2-2 dhidi ya Ruvu Shooting ya mkoani Pwani.
Mabao ya Ashanti yalifungwa na Tumba Swedi dakika ya nane kwa penalti na Mussa Nampaka dakika ya 88, wakati ya Ruvu yote yalifungwa Elias Maguri dakika za 24 na 49.
Afisa habari wa Shooting, Masau Bwire ameumbia mtandao huu kuwa walianza kufunga mabao mawili na baadaye wachezaji wao waliridhika na kujikuta yanasawazisha.
“Kocha Charles Mkwasa anaenda kuwaambia wachezaji wake waache tabia ya kuridhika kabla ya dakika 90, kiukweli tulikuwa tunashinda huu mchezo, lakini wameshindwa kuwa makini, lazima uzembe huu utupiwe macho na makocha”. Alisema Masau.
Na mechi ya mwisho ilikuwa huko Kaitaba mkaoni Kagera ambapo Wageni wa uwanja huo Coastal Union ya Tanga wameendelea kukalia kiti cha moto baada ya kukubali kipigo cha bao 1-0 kutoka kwa wana `Nkulukumbi` Kagera Sugar. Bao pekee limefungwa na Salum Kanoni kwa penalti dakika ya 58.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video