Na Waitara Meng’anyi, Tarime
Ghati
Chacha (21) mkazi wa kijiji cha Nyanitira kata ya Nyansincha Wilayani
Tarime amesababishiwa kilema cha maisha kwa kukatwa mguu wake wa kulia
na Mume wake baada ya kuchelewa kumfungulia mlangao nyakati za usiku.
Akisimulua
mkasa huo hivi karibuni akiwa wodi namba sita alikolazwa akiuguza
vidonda na majeraha,Ghati alisema, mume wake aliyemtaja kwa majina ya
Chacha Mwita(23) alifika nyumbani saa mbili usiku akiwa amelewa.
“Aliniuliza
kwa nini nimechelewa kumfungulia mlango nikamjibu sikuwa nasikia,
baadaye akaniomba kurunzi na panga, nikamletea kurunzi na kumwonesha
panga lilipo kwa kidole” alisema Ghati.
Wakati
anamwonesha lilipo panga na kumpa kurunzi, Ghati hakujuwa kuwa nini
kinafuata, alifikiri kuwa mambo ya wanaume pengine anataka kwenda
sehemu kwa kuwa ndizo tabia za wanaume wa maeneo haya kuondoka usiku ama
anataka kuangalia mji kama uko sawa halafu arudi kulala.
“
Alipoipata ile panga akaniambia leo atanitumbua utumbo, akaanza
kunipiga kwa panga ile akanijeruhi sikio, mkono wa kushoto na mguu wa
kushoto na kunikata mguu wa
kulia ukakatika kama unavyoona” alieleza kwa masikitiko akiifunua kanga iliyokuwa amejifunika akiwa amelala kitandani hospitali ya Wilaya Tarime.
kulia ukakatika kama unavyoona” alieleza kwa masikitiko akiifunua kanga iliyokuwa amejifunika akiwa amelala kitandani hospitali ya Wilaya Tarime.
Wakati
anafanyiwa ukatili huo alipiga kelele lakini majirani hawakuwahi kufika
kumsaidia kwa kuwa ni kawaida ya mume na mke kugombana na vilio kama
hivyo kusikika katika
maeneo hayo.
maeneo hayo.
“Baadaye
walikuja na aliposikia majirani wamefika alikimbia kwa kupitia mlango
wa nyuma akitumia baisikeli yake, majirani walinifunga mguu uliokuwa
ukivuja damu na kunikimbiza katika kituo cha afya Muriba na baadaye
kuletwa hapa” alieleza .
Hata hivyo mwanzoni Ghati alieleza kuwa chanzo cha matatizo hayo yote ni ndoa za mitala na unywaji wa pombe wa mume wake.
“
Nimeishi naye kwa miaka minne sasa na tuna watoto wawili na tulikuwa
tunaishi vizuri, tatizo akinywa pombe huonekana kama amewehuka, lingine
ni baada ya kuoa mke wa pili ambapo alianza kunichukia , kuanza
kunipiga na sasa kunikata mguu” alisema Ghati.
Ghati hataweza kurudiana na mume wake huyo kwa kitendo alichomfanyia kwa vile amesema hakioneshi utu na kuiomba mahakama imuhukumu mumewe kifungo jela ili ajifunze kutokana ukatili aliomfanyia.
”
Naomba serikali na watu binafsi wanisaidie magongo ya kutembelea kwa
kuwa sasa sina uwezo wa kuyanunua pia wanisaidie kusomesha watoto wangu
maana ni wadogo na mimi ndiye niliye kuwa nikitafuta tunakula” alisema.
Wananchi
walioshuhudia kitendo hicho walionesha kusikitishwa na kukilaani kuwa
kinaendelea kuharibu jina na sifa ya Wilaya ya Tarime .
“
Sikifurahii kitendo hiki kwani kinaonesha wazi ukatili wa hali ya juu
kwa binadamu mwenzako na hii inasababisha hata watu ambao hawajawahi
kufika huku kutuona sisi ni
wanyama kumbe ni watu wachache wanaotuharibia sifa, mahakama imuhukumu huyu mtu adhabu kubwa inayomstahili ili liwe fundisho kwa wengine” alisema Mwita Machera aliyekuwa hostalini hapo.
wanyama kumbe ni watu wachache wanaotuharibia sifa, mahakama imuhukumu huyu mtu adhabu kubwa inayomstahili ili liwe fundisho kwa wengine” alisema Mwita Machera aliyekuwa hostalini hapo.
Jeshi
la polisi baada ya kupata taarifa lilifika eneo hilo la tukio na
kushuhudia kipande cha mguu na kuamuru kizikwe na juhudi za kumtia
nguvuni kuanza.
Hata
hivyo siku moja baadaye Chacha Mwita alikamatwa na jeshi la polisi kwa
kusaidiana na nguvu za wananchi ambapo alifikishwa katika mahakama ya
Wilaya ya Tarime kujibu mashitaka hayo.
Akithibitisha
kutokea kwa tukio hilo kamishina masaidizi wa polisi kanda maalumu ya
Tarime (ACP) Justus Kamugisha lisema kuwa baada ya kuhojiwa Mwita
alikiri kumsababishia mke wake ukilema wa maisha.
“
Vitendo vya kikatili vilishapitwa na wakati, kumsababishia mtu ukilema
wa maisha si jambo lisilo la utu na linaonesha kuwa hakuna ubinadamu kwa
watu japo si wote” alisema Kamugisha kwa nija ya simu.
KWA HISANI YA DJ SEK
0 comments:
Post a Comment