Saturday, October 19, 2013

SAM_1032
Kocha wa Coastal Union, Hemed Morroco (wa kwanza kulia) hajafukuzwa na wagosi wa Kaya bali mkataba wake umekwisha
Na Oscar Assenga, Tanga.
MJUMBE wa Kamati ya Utendaji ya Klabu ya Coastal Union ya Tanga, Albert Clement Peter “Mkubwa wa Kazi amekanusha vikali taarifa zilizosambazwa na baadhi vyombo vya habari kuwa wamemfukuza kocha wao mkuu Hemed Morroco.
Akizungumza jana, Peter alisema wao hawajamfukuza kocha huyo kama ilivyoripotiwa bali mkataba wake wa kuendelea kuinoa timu hiyo umekwisha hivyo wataangalia hatima yake kama watamuongezea au la.
Alisema hivi sasa kocha huyo yupo mjini Bukoba akiwa na kikosi cha timu hiyo wakijiandaa na mechi yao dhidi ya Kagera Sugar ambayo itachezwa Jumamosi hii kwenye dimba la soka la Kaitaba.
 “Mimi nashangaa sana kusikia baadhi ya vyombo vikiripoti tumemfukuza Morroco hizo habari wamezitoa wapi jamani acheni uzushi Morroco bado ni kocha wetu na yupo na timu bukoba “Alisema Peter.
Mjumbe huyo alisema uongozi wa klabu hiyo umeshapitisha jina la msemaji wao na hivyo wanatarajia kumtangaza muda wowote ambaye atachukua nafasi ya Edo Kumwembe.
Alisema mkataba wa kocha huyo uliisha tokea mwanzoni mwa mwezi huu ambapo bado uongozi haujakaa naye na kuzungumza kuhusiana na mkataba mpya.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video