Saturday, October 19, 2013

Na Baraka Mpenja , Dar es salaam
WAKATI homa ya pambano la watani wa jadi, Simba Sc na Yanga ikizidi kushika kasi na habari ya mjini ikiwa ni hadithi juu ya mechi hiyo ya kukata na shoka, wadau wazidi kutathmini kipute hicho kitakachopigwa kesho (Octoba 20 mwaka huu) uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.
Asubuhi hii, mtandao wa MATUKIO DUNIANI umekutana uso kwa uso na beki wa zamani wa Yanga na sasa mchambuzi na soka nchini, Ally Mayay Tembele, ambaye kwa upande wake amesema mechi ya kesho ni ngumu kwa timu zote licha ya watu wengi kuamini kuwa wanajangwani wana nafasi kubwa ya kuibuka kidedea kwa madai ya kuwa na kikos imara na kilichodumu kwa muda mrefu.
“Mechi za Simba na Yanga si rahisi kutabiri, unaweza kusema labda Yanga ni bora zaidi ya Simba au Simba ni zaidi ya Yanga, lakini aliyebora zaidi ya mwenzake kwa wakati huo akashindwa kupata matokeo ya uwanjani, kwahiyo ni kusubiri kuona nini kitatokea uwanjani”. Alisema Mayay ambaye alikuwa beki wa zamani wa Yanga.
Mayay aliongeza kuwa kuna wakati Yanga SC waliwahi kufukuza wachezaji takribani wote na wakatumia kikosi B, na Simba SC wakawa na imani kubwa ya kuwafunga, lakini hadi dakika tisini zinamalizika, matokeo yalikuwa sare.
Beki huyo aliyekuwa na sifa ya kucheza soka safi na kukaba kwa akili enzi zake,  aliongeza kuwa kwasasa Yanga wanaonekana kuwa na kikosi kizuri zaidi ya Simba SC na watani wao wana kikosi kizuri pia na kipya achilia mbali wachezaji wachache waliokuwepo mechi iliyopita mei 18 mwaka hii akiwemo Amri Ramadhan Kiemba na Masud Nassor Cholo, lakini katu hawezi kutabiri nani atakuwa mshindi kwani soka la klabu hizo ni gumu kutabiri.
Ally Mayay Tembele waliochuchumaa chini (wapili kulia) enzi zake akiitumika klabu ya Yanga, alikuwa beki makini mno na sasa ni moja kati ya wachambuzi wazuri wa soka la Tanzania.
“Mimi hata ukinikuta njiani, ghafla ukaniuliza, nani ataibuka na ushindi kesho?, sitaweza kukupa utabiri hata kidogo zaidi ya kukwambia tusubiri dakika 90, kwani hizi timu mbili wewe zisikie tu”. Alisema Mayay.
Akizungumzia uzoefu wake alioupata wakati akichezea timu ya Yanga, Mayay alisema wachezaji wanapoingia uwanjani kwenye mechi ya watani wa jadi,  wanatafuta zaidi ya matokeo ya ushindi, kwani wanaingia kwa kukamia ili kuonesha ubora wao kwa mashabiki.
“Zinapokana timu hizi, wachezaji wanajituma zaidi na kuonesha kiwango chao, wanatafuta ushindi kwa nguvu zote kwani ndio sifa yao ukizingatia hizi ndizo klabu kubwa zaidi hapa nchini, binafsi nitaingia uwanjani kwa kusuburi dakika za mwamuzi”. Alisema Mayay.
Wachezaji+wa+Simba+na+Yanga,+wakisalimiana+kabla+ya+kuanza+mchezo+huo 
Katika mchezo wa kesho, Yanga itaingia na wachezaji wengi waliocheza mechi ya mei 18 mwaka huu ya kufunga dimba la ligi kuu soka Tanzania bara ambapo Simba walilala kwa mabao 2-0.
Yawezekana wachezaji kama Ally Mustapha `Bartez`, Mbuyu Twite, Nadir Haroub `Canavaro`, Kelvin Yondan, Athumani Idd `Chuji`, Haruna Niyonzima, Didier Kavumbagu, Jerry Tegete, Hamis Kiiza, Saimon Msuva wataanza,  pia kutakuwa na ongezeke la David Luhende ambaye kwa wakati ule hakuaminiwa kama sasa, atakuwepo Mrisho Ngassa ambaye alikuwa Simba na wengine wengi.
Kikosi cha Simba asilimia kubwa ni wapya na hawakuwepo, mfano ambao hawakucheza na hawakuwepo ni Abel Dhaira, Issa Rashid, Gilbert Kaze, Joseph Owino Gella, Betram Mwombeki, Hamis Tambwe, Henry Joseph, ila  pia watakuwepo vijana waliotoka kikosi B, Harun Chanongo, Jonas Mkude, Ramadha Singano, William Lucian `Gallas` na wengineo.
Baadhi ya wachezaji muhimu wa Simba sc msimu ulipita hawapo, mfano Nahodha wake Juma Kaseja aliyemaliza mkataba na kalbu, Juma Nyoso, Haruna Moshi `Boban` wote wapo coastal Union, Amir Maftah, Emmanuel Okwi, Ferlix Sunzu, Musa Mude, Shomary Kapombe na wengineo.
Kwahiyo unaweza kusema Simba sc mpya inaenda kukabiliana na Yanga ileile ya Zamani, dakika 90 zinasubiriwa kwa hamu kubwa kuona nani ataibuka na pointi tatu muhimu kwenye mchezo wa kesho..

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video