Na Baraka Mpenja, Mbeya
HOMA
ya pambano la jumamosi baina ya Mbeya City dhidi ya mabingwa wa ligi
kuu soka Tanzania bara, klabu ya Yanga katika uwanja wa sokoine jijini
hapa inazidi kupanda moto huku kila kona hadithi kubwa ikiwa ni mechi
hiyo.
Wakati
mechi hiyo inazidi kutawala midomoni mwa watu, vijana wa Mbeya City
wanazidi kujiimarisha zaidi kuelekea mchezo huo ambapo wanaendelea na
mazoezi yao katika uwanja wa sokoine chini ya kocha Juma Mwambusi.
Mwambusi
mwenye uzoefu na ligi kuu itaiongoza timu yake hiyo ambayo ni mara ya
kwanza kukabiliana na Yanga, huku akiwa na matumaini ya kuwaadabisha
wana jangwani hao wanaotamba kuwa timu bora na mabingwa watarajiwa wa
ligi kuu msimu wa 2013/2014.
“Tunawaheshimu
sana Yanga, ni klabu kubwa na yenye uzoefu mkubwa, lakini sisi
tumejiandaa kucheza na timu zote 13, hivyo hatujali kama ni Yanga au
nani, kikubwa tuko vizuri na tunahitaji ushindi ili kuendelea kujiweka
sehemu nzuri”. Alisema Mwambusi baada ya mazoezi ya timu yake.
Wakati
huo huo kikosi cha wanajangwani chini ya kocha wake, Mholanzi, Ernie
Brandts kinatarajiwa kuwasili leo jijini Mbeya tayari kwa mawindo yake
ya mechi hiyo yenye mvuto wa aina yake kwa mashabiki wa kandanda.
Wachezaji ambao wapo safarini ni Makipa: Ally Mustafa ‘Barthez’, Deogratius Munishi ‘Dida’ na Yusuph Abdul,.
Walinzi:
Juma Abdul, David Luhende, Nadir Haroub `Cannavaro`, Mbuyu Twite,
Oscar Joshua, Kevin Yondan, Rajab Zahir , Issa Ngao na Ibrahim Job.
Viungo
ni Athuman Idd ‘Chuji’, Salum Telela, Frank Domayo, Haruna Niyonzima
`Fabregas`, Nizar Khalfani, Hamisi Thabit na Bakari Masoud.
Wakati
washambuliaji ni Simon Msuva, Mrisho Ngassa, Abdallah Mguhi, Didier
Kavumbagu, Jerry Tegete, Hussein Javu, Said Bahanuzi, Shaban Kondo na
Reliants Lusajo.
Mbeya
City tayari wameshashuka dimbani mara mbili katika uwanja wao wa
nyumbani ambao mechi ya kwanza ilichezwa agosti 24 dhidi ya Kagera Sugar
na walitoka suluhu, huku mechi ya pili wakishinda mabao 2-1 dhidi ya
Ruvu Shooting.
Nao
Yanga wamekipiga mara mbili huku mechi ya kwanza wakishinda kwa mabao
5-1 dhidi ya Ashanti United, na mechi ya pili wakatoka sare ya 1-1 dhidi
ya Coastal Union.
0 comments:
Post a Comment