Tuesday, September 10, 2013

Na Baraka Mpenja , Mbeya
HAKIKA mkubwa ni mkubwa tu!, mpaka sasa mashabiki wa soka jijini Mbeya wameshashuhudia mechi mbili za ligi kuu soka Tanzania bara msimu huu wa 2013/2014 ambapo mechi ya kwanza iliwakutanisha Mbeya City dhidi ya Kagera Sugar, huku ya pili wakicheza na Ruvu Shooting, lakini ujio wa Mabingwa watetezi, klabu ya Yanga ya Dar es salaam umebadili hali ya hewa jijini hapa.
Kila kona ya jiji la Mbeya, gumzo zito limetawala kwa mashabiki wa kandanda kuzungumzia mtanange huo wa kukata na shoka utakaopigwa siku ya jumamosi Septemba 14 baina ya Wenyeji Mbeya City na Yanga huku ikiwa mara ya kwanza kwa wakali hao wa Mbeya kukutana na presha ya timu kubwa na kongwe katika soka la Tanzania.
Pambano hilo limevuta hisia za mashabiki wengi ukizingatia Yanga ni klabu kubwa yenye mashabiki kila kona ya Tanzania, hivyo mechi zake zinakuwa na msisimko mkubwa kama ilivyo kwa wekundu wa Msimbazi Simba ambao siku hiyo watakuwa na kibarua kizito mbele ya Mtibwa Sugar, uwanja wa Taifa jiijini Dar es salaam.
DSC00055
Kocha wa Mbeya City, Juma Mwabusi akiongea na waandishi wa habari
Mtandao huu umefanikiwa kutembelea mazoezi ya klabu ya Mbeya City yanayoendelea katika dimba la Sokoine jijini hapa na kujionea mikakati mizito ya benchi la ufundi kuhakikisha wanashinda mechi hiyo iliyopandisha homa ya wapenda soka kila kona ya mji.
Akizungumza katika mazoezi hayo, kocha mkuu wa klabu hiyo, Juma Mwambusi amesema vijana wake wanaendela vizuri na wapo katika morali kubwa ya kuwakabili wanajangwani waliosheheni nyota wengi wakiwemo, Jerryson Tegete, Haruna Niyonzima “Fabregas”, Didier `Kavu` Kavumbagu, Mbuyu Twite, Frank Domayo, Nadir Haroub `Canavaro` ,  n.k.
“Sisi tunajiandaa na mechi ijayo bila kujali ni Yanga, tukisema tunajiandaa na Yanga tunaonesha kuwa klabu hiyo ni tofauti na timu nyingine. Tunawaheshimu sana, ni timu kubwa, kongwe na yenye uzoefu mkubwa, lakini sisi tumejiandaa kucheza na timu zote 13 za ligi kuu msimu huu wa ligi”. Alisema Mwambusi.
Mwambusi amewataka mashabiki wa Mbeya City kuamini kuwa wanaweza kushinda mechi hiyo bila kujali ubora wa Yanga, hivyo lazima wajitokeze kwa wingi kuishangilia timu yao inayovuta hisia za mashabiki wengi jijini Mbeya.
DSC_0352 
Mbeya City ni klabu ya wananchi na ina mashabiki lukuki, sasa sijui jumamosi itakuwaje uwanjani, kwani mwaka jana Yanga ilikuwa na mashabiki wengi zaidi ya Prisons zilipokutana uwanja wa Sokoine. IMG_8317 
Wakati hayo yakijiri, naye meneja wa uwanja wa sokoine, Modestus Mbande Mwaluka anaendelea kuufanyia ukarabati uwanja wake kwa kumwagilia maji, kuweka uzio wa nguvu ili kujihami na hali ya mashabiki kuingia uwanjani kinyume na taratibu zilizowekwa.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video