Friday, September 27, 2013


Na Baraka Mpenja , Mbeya
 MIKIKIMIKIKI ya ligi kuu soka Tanzania bara msimu wa 2013/2014 inatarajiwa kuendelea kushika kasi wikiendi hii (Jumamosi na jumapili), huku macho ya mashabiki wengi wa soka wakisubiri kuona nini mabingwa watetezi, Klabu ya Yanga watafanya dhidi ya Ruvu Shooting Uwanja wa Taifa  baada ya kukubali kichapo cha mabao 3-2 wiki iliyopita kutoka kwa Azam Fc.
Yanga wanatarajiwa kushuka dimbani hapo kesho (septemba 28) katika dimba lao la nyumbani dhidi ya vijana wa Charles Boiface Mkwasa `Master`, huku wakiwa na pointi 6 tu katika nafasi ya 8 ya msimamo.
Wanajangwani wataingia uwanjani wakiwa na machungu ya kufanya vibaya mechi za nyuma na tayari mwenyekiti wa klabu hiyo, Yufus Manji amewataka wachezaji kutulia na kuwasisitiza kuwa hana tatizo nao kutoakana na matokeo mabaya.
12 
DSC_0153 

Sakata la Ngassa lilianzia Agosti mwaka jana alipoupandisha hasira uongozi wa iliyokuwa klabu yake, Azam FC kwa kwenda kubusu jezi ya Yanga SC baada ya kufunga bao la ushindi katika Nusu Fainali ya Kombe la Kagame dhidi ya AS Vita ya DRC, Uwanja wa Taifa.
51e4Ismail-Aden-Rage 
Mwenyekiti wa Simba Sc, Aden Rage hataki fedha za mafungu mafungu kutoka kwa Ngassa

Wakati huo huo, Uongozi wa Simba Sc kupitia kwa mwenyekiti wake, Alhaj Ismail Aden Rage umetoa msimamo wake kuwa Ngassa anatakiwa kulipa fedha zote na hawako tayari kupokea kwa mafungu mafungu kama walivyofanya wakati wa sakata la Mbuyu Twite.
Rage ametoa tahadhari hiyo huku akisema wao wanapenda nyota huyo acheze soka, lakini wanataka mzigo wote na si nusu nusu, vinginevyo hawatakubali.
Lakini amesisitiza kuwa Ngassa hajaomba kulipa kwa mafungu, ila wamelazimika kutoa msimamo huo kwani fedha ya mafungu mafungu huwa zinatibua bajeti yao kama ilivyotokea kwa mzigo waliolipwa na Yanga wakati wa sakata la beki Mbuyu Twite aliyekula fedha za Simba na kisha kusaini Yanga.
DSC00068 
Kikosi cha Mbeya City
Mbali na mechi hiyo, kipute kingine cha kuvutia kitakuwepo katika dimba la Sokoine hapa jijini Mbeya ambapo wakali wanaotikisa na kugonga akili za wapenzi wengi wa soka nchini, klabu ya Mbeya City itakuwa kibaruani kumenyana na Wagosi wa Kaya, Coastal Union ya Tanga.
City waliopo nafasi ya 7 wakijikusanyia pointi 7 watashuka dimbani mbele ya Wagosi wa Kaya wenye pointi 9 katika nafasi ya 5 ili kusaka ushindi wa pili uwanja wa nyumbani.
Ikumbukwe kuwa hiyo itakuwa mechi ya nne kwa Mbeya City kucheza nyumbani, ambapo alianza mechi ya ufunguzi na Kagera Sugar, ikacheza na Ruvu Shooting na hatimaye na Yanga kabla ya kwenda Manungu kucheza na Mtibwa Sugar na kuingia Dar es salaam kukipiga na Simba.
Kati ya mechi hizo za nyumbani ilishinda moja tu dhidi ya Ruvu shooting kwa mabao 2-1 na nyingine iliambulia suluhu na sare.
Huko  uwanja wa A.H. Mwinyi, Maafande wa jeshi la wananchi (JWTZ), Rhino Rangers watakuwa wenyeji wa `Wanankulukumbi`, Kagera Sugar.
Mechi nyingine itawakutanisha Mgambo JKT katika dimba la Mkwakwani dhidi ya Maafande wa jeshi la kujenga Taifa, JKT Oljoro kutoka mjini Arusha.
Mitanange ya Ligi hiyo itaendelea jumapili kwa mechi tatu kupigwa katika viwanja Tofauti.
Vinara wa ligi hiyo wenye pointi 11, wekundu wa Msimbazi Simba watakuwa ugenini katika dimba la Taifa jijini Dar es salaam kukabiliana na maafande wa JKT Ruvu FC waliopo nafasi ya pili wakiwa na pointi 9 kibindoni.
mwombeki 
Nao vibonde Ashanti United watakuwa kibaruani kupepetana na Mtibwa Sugar uwanja wa Azam Complex.
Maafande wa Tanzania Prisons `Wajelajela` watakuwa mzigoni kusaka pointi tatu muhimu mbele ya wana Lambalamba, Azam C katika uwanja wa Soine jijini Mbeya.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video