Tuesday, September 24, 2013

CAG Ludovick Utouh 
Na Benedict Liwenga-Maelezo, Dar es Salaam.
SERIKALI inayoendesha mambo yake kwa uwazi inatimiza sharti la msingi la utawala bora kwa kuwajibika ipasavyo kwa wananchi wake.
Hayo yamesemwa leo na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali Bw. Ludovick Utouh wakati wa ufunguzi wa Warsha ya siku moja kwa vyombo vya habari na asasi za kiraia kuhusu utekelezaji wa mapendekezo ya CAG na kuelewa ripoti za Mdhibiti Mkuu wa hesabu za serikali.
Bw. Utouh amesema kuwa kutokana na ongezeko la matumizi ya ripoti zake kwa vyombo vya habari na wadau wengine kumekuwa na upotoshwaji mkubwa wa taarifa kwa namna zinavyotumiwa na wadau mbalimbali, hivyo warsha hiyo inatoa fursa ya pekee ili kupunguza upotoshwaji huo kwa kuelimishana, kurekebishana na kusaidiana ili kuzielewa vizuri ripoti hizo na kuzilipoti kwa usahihi.
“Warsha hii inalenga kutoa fursa ya kipekee kwa wadau wetu kushiriki na kutoa mawazo yao ya namna ya kuboresha mahusiano ambayo yataleta ufumbuzi na wa madai mbalimbali vikiwemo vyombo vya habari na asasi mbalimbali”. Alisema Bw. Utouh.
Bw. Utouh ameongeza kuwa ni vema kufahamu madhara juu ya utoaji taarifa za upotoshwaji ili kuepusha madhara ambayo yanaweza kujitokeza baina ya pande mbili na pia amesema kuwa ana imani kubwa kuwa kila mwanahabari anatambua umuhimu wa habari na pia kutambua umuhimu wa uwajibikaji na utawala bora.
“Msiweke madoido, msipambe taarifa ili kwamba zionekane zina mvuto”. Alisisitiza Bw. Utouh.
Aidha, Bw. Utouh amevitaka vyombo vya habari kwa kushirikiana na asasi za kiraia kwa pamoja kuhakikisha kuwa kuna mfumo mzuri wa upatakinaji wa taarifa na utaoji wa taarifa za serikali kwa usahihi.
Warsha hiyo imefunguliwa leo Landmark Hotel iliyoko Mbezi Beach jijini Dar es Salaam na inalenga kuwajengea uwezo maafisa habari nchini juu ya kazi za Mdhibiti wa Hesabu za Serikali na juu ya ubora wa upatikanaji wa habari zilizosahihi na kuziripoti kwa usahihi.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video