Wednesday, September 25, 2013

 Wanajeshi watatu wa Kenya wameuawa wakati walipokuwa wakijaribu kuokoa maisha ya watu anaoshikiliwa mateka na magaidi wa al Shabab katika jumba lenye maduka la Wastgate jijini Nairobi.
Askari wengine 8 wanaripotiwa kuwa mahututi baada ya kujeruhiwa katika mapambano hayo yanayoendelea hadi sasa.
Hayo yamesemwa na Mkuu wa Jeshi la Ulinzi la Kenya (KDF) Jenerali Julius Karangi.
Duru za Kenya zinaripoti kuwa hadi sasa watu 69 wamethibitishwa kuwa wameuawa na magaidi wanaoendelea kupigana na vikosi vya jeshi la Kenya katika jengo la maduka la Westgate.
Wakati huo huo Waziri wa Mambo ya Nje wa Kenya Balozi Amina Mohammed amesema kuwa Wamarekani wawili au watatu na Mwingereza mmoja wamehusika katika shambulizi lililofanywa na magaidi dhidi ya jumba la maduka la Westgate jijini Nairobi. Balozi Amina Mohammed amesema washambuliaji hao walikuwa wakishirikiana na wenzao katika maeneo mbalimbali ya dunia kwa ajili ya kuua watu mwishoni mwa wiki mjini Nairobi. Waziri wa Mambo ya Nje wa Kenya amesisitiza kuwa shambulizi la sasa mjini Nairobi limefanyika kitaalamu.
CHANZO: RADIO TEHRAN

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video